1Kisha nikaona mbingu mupya na dunia mupya. Kwa sababu mbingu ya kwanza na dunia ya kwanza vilikuwa vimekwisha kutoweka, bahari nayo haikukuwa tena.
2Nikaona muji mutakatifu, ndio Yerusalema mupya, uliokuwa ukishuka toka mbinguni kwa Mungu, nao ukitengenezwa vizuri kama vile bibi arusi aliyepambwa kwa ajili ya kwenda kukutana na mume wake.
3Nikasikia sauti kubwa tokea kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa makao ya Mungu yanapatikana kati ya watu! Yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao.
4Yeye atapanguza machozi yao yote na kifo hakitakuwa tena, wala kilio, wala malalamiko, wala maumivu. Kwa maana dunia ya mbele imekwisha kupita.”
5Basi yule aliyekuwa akiikaa juu ya kiti cha kifalme akasema: “Angalia ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Kisha akaniambia: “Andika maneno haya, kwa maana ni ya kweli na ya uhakika.”
6Akasema tena: “Sasa ni mwisho! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Yule anayesikia kiu, nitamupa maji ya kunywa yanayotoka katika chemichemi ya maji ya uzima pasipo kulipa.
7Yule atakayeshinda atapokea toka kwangu zawadi ile, mimi nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwana wangu.
8Lakini watu wenye woga, wasioamini, wenye machukizo, wauaji, wazinzi, wachawi, wanaoabudu sanamu na wote wanaosema uongo, fungu lao ni katika lile ziwa la moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto. Hiki ndicho kifo cha pili.”
Yerusalema mupya9Kisha mumoja wa wale wamalaika saba walioshika vile vikombe vilivyojaa mapigo saba ya mwisho, akajongea na kuniambia: “Kuja nitakuonyesha bibi arusi, muke wa Mwana-Kondoo.”
10Nikashikwa na Roho, na malaika akanipeleka juu ya mulima mukubwa na murefu. Akanionyesha muji mutakatifu, ndio Yerusalema uliokuwa ukishuka toka mbinguni kwa Mungu,
11nao ukingaa kwa utukufu wa Mungu. Mwangaza wake ulikuwa kama jiwe la bei kali la yaspi, linalongaa kama kioo.
12Ulikuwa ukizungukwa na ukuta mukubwa na murefu wenye milango kumi na miwili na wamalaika kumi na wawili walichunga milango ile. Na juu ya milango ile, kulikuwa kumeandikwa majina ya makabila kumi na mawili ya Waisraeli.
13Kila upande kulikuwa milango mitatu: upande wa mashariki milango mitatu, upande wa kaskazini milango mitatu, upande kusini milango mitatu na upande wa magaribi milango mitatu.
14Na ukuta uliozunguka muji ule ulikuwa umejengwa juu ya mawe ya musingi kumi na mawili na juu ya kila jiwe kulikuwa kumeandikwa jina la kila mumoja wa mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.
15Malaika yule aliyekuwa akisema nami alikuwa na fimbo ya kupima ya zahabu kusudi apate kupima muji ule, milango yake na ukuta unaouzunguka.
16Muji ule ulikuwa umejengwa namna ya muraba, urefu wake na upana wake vilikuwa sawasawa. Malaika akapima muji ule na ile fimbo; ulikuwa na urefu, upana na urefu wake wa kwenda juu yapata kilometre elfu mbili na mia ine.
17Malaika akapima vilevile ukuta; ulikuwa yapata metre makumi sita kufuatana na kipimo cha kawaida cha wanadamu ambacho yule malaika alichotumia.
18Ukuta ulikuwa umejengwa na mawe ya bei kali ya yaspi, na muji wenyewe ulikuwa umejengwa na zahabu safi inayongaa kama kioo.
19Musingi wa ukuta uliozunguka muji ule ulikuwa unapambwa na mawe ya bei kali ya kila aina. Mawe ya musingi wa kwanza ulikuwa wa mawe ya yaspi, wa pili wa mawe ya safilo, wa tatu wa mawe ya kaledoni, wa ine wa mawe ya zumaridi,
20wa tano wa mawe ya sadoniki, wa sita wa mawe ya akiki, wa saba wa mawe ya krisolite, wa nane wa mawe ya belulo, wa tisa wa mawe ya topazo, wa kumi wa mawe ya krisoparazo, wa kumi na moja wa mawe ya haikinto na wa kumi na mbili wa mawe ya amazito.
21Na ile milango kumi na miwili ilikuwa ushanga nzuri kumi na mbili; kila mulango ulikuwa umetengenezwa na ushanga moja. Barabara ya muji ule ilikuwa imetengenezwa na zahabu safi inayongaa kama kioo.
22Sikuona hekalu ndani ya muji ule, maana Bwana wetu Mungu Mwenye Uwezo na yule Mwana-Kondoo ndio hekalu lake.
23Muji ule hauna lazima ya mwangaza wa jua, wala wa mwezi, kwa sababu utukufu wa Mungu unauangazia na Mwana-Kondoo ndiye taa yake.
24Kwa hiyo watu wa mataifa watatembea katika mwangaza wake na wafalme wa dunia wataleta utajiri wao ndani yake.
25Milango ya muji ule haitafungwa muchana maana ndani yake hakutakuwa usiku.
26Heshima na utukufu za watu wote wa mataifa zitaletwa ndani ya muji ule.
27Hakuna kitu chochote kichafu kitakachoingia ndani yake, wala yeye anayefanya machukizo na kusema uongo; lakini wale tu ambao majina yao yaliandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.