1 Yoane 2 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kristo ndiye muteteaji wetu mbele ya Mungu

1Watoto wangu wapendwa, ninawaandikia maneno hayo kusudi musitende zambi. Lakini kama mutu akitenda zambi, tuko na yule anayetutetea mbele ya Baba. Naye muteteaji yule ndiye Yesu Kristo, mwenye haki.

2Yeye ndiye sadaka iliyotolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu, wala si kwa ajili ya zambi zetu tu, lakini kwa ajili ya zambi za watu wote.

3Sisi tunatambua kwamba tunamujua Mungu ikiwa tunashika amri zake.

4Mutu akijidai kwamba anamujua Mungu, lakini hashiki amri zake, yeye ni mwongo, nao ukweli hauko ndani yake.

5Lakini yule anayetii neno la Mungu yuko na upendo kamili wa Mungu ndani yake. Hili ndilo jambo linalotuonyesha kwamba sisi tunaungana na Mungu:

6mutu yeyote anayesema kwamba anaungana na Mungu anapaswa kuishi sawa vile Yesu alivyoishi.

Amri mupya

7Wapenzi, siwaandikii amri mupya, lakini ile ya zamani muliyoijua tangia mbele. Na amri hiyo ya zamani ni lile neno mulilosikia.

8Kwa ngambo ingine amri hii ninayowaandikia ni mupya, na ukweli wake unaonekana ndani ya Kristo na ndani yenu vilevile. Kwa maana giza linapita na mwangaza wa kweli umekwisha kutokea.

9Mutu anayesema kwamba anaishi katika mwangaza, lakini anamuchukia ndugu yake, yeye angali anaishi katika giza.

10Yule anayemupenda ndugu yake, anaishi katika mwangaza na ndani yake hamuna kitu kinachoweza kuangusha mwingine katika zambi.

11Lakini anayemuchukia ndugu yake anaishi na kutembea katika giza, wala hajui pahali anapokwenda kwa sababu giza limemupofusha macho.

12Ninawaandikia ninyi watoto wangu, kwa sababu mumesamehewa zambi zenu kwa jina la Kristo.

13Ninawaandikia ninyi wababa, kwa sababu mumemujua yule aliyekuwa tangu mwanzo wa vitu vyote. Ninawaandikia ninyi vijana kwa sababu mumemushinda yule Mwovu.

14Nimewaandikia ninyi watoto, kwa sababu mumemujua Baba. Ninawaandikia ninyi wababa, kwa sababu mumemujua yule aliyekuwa tangia mwanzo wa vitu vyote. Ninawaandikia ninyi vijana, kwa sababu muko na nguvu na Neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mumemushinda yule Mwovu.

15Musipende dunia, wala mambo yanayokuwa katika dunia. Mutu akipenda dunia, hawezi kumupenda Mungu Baba.

16Kwa maana kila kitu kinachokuwa katika dunia, kama vile tamaa ya kimwili, tamaa ya macho, na majivuno ya maisha, hivi vyote havitoki kwa Baba, lakini vinatoka katika dunia.

17Dunia inapita pamoja na tamaa zake, lakini mutu yule anayefanya mapenzi ya Mungu anaishi milele.

Adui wa Kristo

18Watoto wangu, huu ni wakati wa mwisho. Mulisikia habari kwamba mupinga Kristo atakuja, lakini hata sasa wapinga Kristo wengi wametokea. Na kwa hiyo tunajua kwamba ni wakati wa mwisho.

19Watu hawa wametoka kati yetu, lakini hawakukuwa wa kundi letu, na kwa sababu hii wametuacha. Kama wangekuwa wa kundi letu, wangekaa pamoja nasi. Lakini wametuacha kusudi ionekane wazi ya kama hawakukuwa wa kundi letu.

20Lakini munajazwa na Roho Mutakatifu ambaye Kristo alimimia juu yenu, na kwa hiyo ninyi wote munajua ukweli.

21Basi, sikuwaandikia kwa sababu hamujui ukweli, lakini kwa sababu munaujua na tena kwa sababu hakuna uongo wowote unaoweza kutokana na ukweli.

22Ni nani anayekuwa musema uongo? Ni yule anayekana kwamba Yesu si Kristo. Huyu ndiye mupinga Kristo, kwa maana anamukana Baba na Mwana.

23Yule anayemukana Mwana, anamukana Baba vilevile, lakini yule anayemukubali Mwana, anamukubali Baba vilevile.

24Kwa hiyo muchunge ndani ya mioyo yenu mafundisho muliyosikia tangia mbele. Kama mukichunga mafundisho yale muliyosikia tangia mbele, mutakaa ndani ya Mwana pamoja na Baba.

25Na Kristo yeye mwenyewe alituahidi sisi uzima wa milele.

26Nimewaandikia maneno hayo kwa sababu ya watu wanaotafuta kuwadanganya.

27Lakini Kristo amemimia Roho juu yenu. Na kufuatana na vile Roho yule anavyokaa ndani yenu, hamuhitaji kufundishwa na mutu, kwa maana Roho wake anawafundisha mambo yote. Roho yule anasema ukweli wala hasemi uongo. Basi kama vile Roho alivyowafundisha, mukae ndani ya Kristo.

28Na sasa watoto wangu, mukae ndani yake kusudi tukuwe na tumaini hakika wakati atakapotokea, na kutosikia haya mbele yake siku atakaporudi.

29Munajua kwamba Kristo ni mwenye haki, kwa hiyo munapaswa kujua vilevile kwamba kila mutu anayefuata haki ni mutoto wa Mungu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help