1Haleluia!
Enyi watumishi wa Yawe, musifu jina lake!
2Jina lake litukuzwe,
sasa na hata milele.
3Kutoka mashariki na hata magaribi,
litukuzwe jina la Yawe!
4Yawe anatawala juu ya mataifa yote,
utukufu wake unafika juu ya mbingu.
5Nani anayekuwa kama Yawe, Mungu wetu?
Yeye anakaa juu kabisa;
6lakini anachungulia chini,
aangalie mbingu na dunia.
7Anamwinua muzaifu toka katika mavumbi,
anamunyanyua mukosefu toka yalala,
8na kumuweka pamoja na wakubwa,
pamoja na wakubwa wa watu wake.
9Anamurudishia heshima mwanamuke anayekuwa tasa;
anamufurahisha kwa kumujalia watoto.
Haleluia!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.