1Nyuma ya hayo, Nahasi mufalme wa Waamoni akakufa, na mwana wake Hanuni akatawala kwa pahali pake.
2Basi, Daudi akasema: “Nitamutendea mema Hanuni mwana wa Nahasi, maana baba yake alinitendea mema vilevile.” Halafu Daudi akatuma wajumbe na kumupelekea salamu za pole kwa ajili ya kifo cha baba yake.
Nao wakaenda kwa Hanuni kwa kumufariji, kule katika inchi ya Waamoni.
3Lakini viongozi wa Waamoni wakamwambia mufalme: “Unazani ni kwa sababu ya heshima ya baba yako ndiyo maana Daudi anatuma wajumbe hawa wakuje kukufariji? Watu hawa ni wapelelezi waliotumwa kuja kuichunguza inchi kwa kuiangamiza na kuipeleleza.”
4Basi Hanuni aliwatwaa wajumbe wale wa Daudi, akawanyoa ndevu na kupasua nguo zao katikati mpaka kwenye matako, kisha akawaacha waende zao,
5nao wakaondoka na kurudi kwao. Daudi alipopashwa habari jinsi wajumbe wake walivyotendewa, akatuma watu kwa kuwapokea maana wale wajumbe waliona haya sana. Naye mufalme akawaambia: “Mukae katika muji wa Yeriko, mpaka mutakapoota ndevu, kisha murudi.”
6Waamoni walipoona wamejifanya wachukizwe na Daudi, Hanuni na wale Waamoni wakatuma watu wapeleke kilo elfu makumi tatu za feza kwa kulipa magari ya vita na waaskari wapanda-farasi kutoka Mesopotamia, Aramaka na Zoba.
7Walikopesha magari elfu makumi tatu na mawili, na mufalme wa Maka na waaskari wake akakuja na kupiga kambi karibu na Medeba. Waamoni walikusanyika toka kwenye miji yao yote, wakajiweka tayari kwa vita.
8Naye Daudi aliposikia habari hizo akatuma Yoabu na kundi lote la waaskari mashujaa.
9Waamoni wakatoka na kujipanga kwenye mulango wa muji, wakati wale wafalme waliokuja walikuwa peke yao kwenye mbuga.
10Yoabu alipoona kwamba vita ni kali juu yake, mbele na nyuma, akachagua waaskari hodari zaidi kati ya Waisraeli, akawapanga mbele ya Waaramu.
11Wale waaskari wengine waliobaki, akawaweka chini ya uongozi wa ndugu yake Abisai, naye akawapanga waangaliane na Waamoni.
12Yoabu akamwambia Abisai: “Ikiwa Waaramu wananizidi nguvu, utanisaidia; lakini kama Waamoni wanakuzidi nguvu, nitakuja kukusaidia.
13Basi ukuwe hodari! Tupigane kama wanaume kwa ajili ya watu wetu, na kwa ajili ya miji ya Mungu wetu; na Yawe atutendee sawa na mapenzi yake.”
14Basi, Yoabu na watu wake walisonga mbele kwa kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia.
15Waamoni walipoona Waaramu wamekimbia, nao walimukimbia Abisai, ndugu ya Yoabu, wakaingia katika muji. Halafu Yoabu akarudi Yerusalema.
16Lakini Waaramu walipoona kwamba wameshindwa na Waisraeli, wakatuma wajumbe waende kuwaleta Waaramu wengine waliokuwa ngambo ya muto Furati wakiongozwa na Sofaki, jemadari wa jeshi la Hadadezeri.
17Daudi alipopata habari, akakusanya pamoja Waisraeli wote, akavuka muto Yordani, akawaendea, akapanga vikundi vyake mbele yao. Daudi alipopanga vita juu ya Wasuria, basi nao wakapigana naye.
18Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Waisraeli. Daudi akawaua Waaramu wanaoendesha magari elfu saba na waaskari wa miguu elfu makumi ine. Vilevile akamwua Sofaki, jemadari wa jeshi lao.
19Kisha watumishi wa Hadadezeri walipoona kwamba wameshindwa na Waisraeli, wakafanya mapatano ya amani na Daudi nao wakakuwa watumishi wa Daudi. Halafu Waaramu hawakukubali kuwasaidia Waamoni tena.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.