2 Mambo ya Siku 23 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Atalia anapinduliwa(2 Fal 11.4-16)

1Katika mwaka wa saba kuhani Yoyada akajipa moyo akafanya mapatano na majemadari: Azaria mwana wa Yoramu, Isimaeli mwana wa Yohanani, Azaria mwana wa Obedi, Maseya mwana wa Adaya, na Elisafati mwana wa Zikiri.

2Wakazunguka katika miji yote ya Yuda wakiwakusanya Walawi na viongozi wa makabila ya Israeli, wakaenda mpaka Yerusalema.

3Mukutano wote ukafanya agano na mufalme katika nyumba ya Mungu. Yoyada akawaambia: “Muangalie huyu mwana wa mufalme! Mumwache atawale kulingana na ahadi Yawe aliyotoa juu ya uzao wa Daudi. Ang. 2 Sam 7.12

4Hivi ndivyo mutakavyofanya: sehemu moja ya tatu ya kundi lenu ninyi makuhani na Walawi mutakaoshika zamu siku ya Sabato, mutalinda milango,

5sehemu moja ya tatu ingine italinda nyumba ya kifalme na sehemu iliyobakia mutalinda Mulango wa Musingi. Watu wote watakuwa katika viwanja vya nyumba ya Yawe.

6Asikubaliwe mutu mwingine yeyote kuingia ndani ya nyumba ya Yawe isipokuwa makuhani tu pekee na wale Walawi watakaokuwa wanatumika. Hao wanaweza kuingia kwa sababu wao ni watakatifu, lakini wale watu wengine wote, watatii amri ya Yawe.

7Walawi watamuzunguka mufalme, kila mutu na silaha yake katika mukono; na mutu yeyote atakayejaribu kuingia katika nyumba ya Yawe, atauawa. Mukae na mufalme anapoingia ndani na anapotoka inje.”

8Walawi na watu wa Yuda walitii amri zote kuhani Yoyada alizotoa. Kila mukubwa akawatwaa watu wake wote, wale waliokuwa wamemaliza zamu na wale waliokuwa wanaingia kushika zamu siku ya Sabato; kwa sababu Yoyada hakuwaruhusu waondoke.

9Kisha kuhani Yoyada akawapa majemadari mikuki na ngao kubwa na ndogo zilizokuwa mali ya mufalme Daudi, na ambazo zilikuwa zimewekwa katika nyumba ya Yawe.

10Kisha, akawapanga watu wote kuanzia upande wa kusini mpaka upande wa kaskazini wa nyumba na kuzunguka mazabahu na nyumba, kila mumoja silaha yake katika mikono, kwa kumulinda mufalme.

11Halafu wakamutoa mwana wa mufalme inje wakamuvalisha taji juu ya kichwa, na kumupa ule ushuhuda; wakamuweka kuwa mufalme nao Yoyada na wana wake wakamupakaa mafuta kisha watu wakashangilia wakisema: “Mufalme aishi milele!”

12Naye Malkia Atalia aliposikia sauti za watu wakikimbia na kumushangilia mufalme akawaendea hao watu waliokuwa katika nyumba ya Yawe.

13Alipochungulia akamwona mufalme mupya akisimama karibu na nguzo kwenye mulango, wakati majemadari na wapiga baragumu wakiwa kando ya mufalme na wakaaji wote wakishangilia na kupiga baragumu; nao waimbaji wakiwa na ala zao za muziki wakiongoza watu katika sherehe; halafu akapasua nguo yake na kusema kwa sauti kubwa: “Uasi! Uasi!”

14Kisha kuhani Yoyada akawatoa inje majemadari wa jeshi akisema: “Mumutoe Atalia inje katikati ya waaskari; yeyote atakayemufuata auawe kwa upanga,” kwa sababu hakutaka wamwue katika nyumba ya Yawe.

15Basi, wakamukamata, na akaingia katika njia ya mulango wa Farasi wa nyumba ya kifalme, wakamwua huko.

Matengenezo ya Yoyada(2 Fal 11.17-20)

16Yoyada akafanya agano kati yake mwenyewe, watu wote, na mufalme kwamba watakuwa watu wa Yawe.

17Halafu watu wote wakaenda kwenye nyumba ya Bali na kuibomoa wakavunja mazabahu pamoja na sanamu zake, hata wakamwua Matani, kuhani wa Bali, mbele ya mazabahu.

18Kuhani Yoyada akaweka walinzi kwa kulinda nyumba ya Yawe. Hao walinzi wakasimamiwa na makuhani na Walawi ambao Daudi aliwaweka katika kazi ya kutunza nyumba ya Yawe kutoa sadaka za kutetezwa kwa moto kwa Yawe kama vile ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, wakishangilia na kuimba kwa kufuata amri ya Daudi. Vilevile wakasimamia mambo ya uimbaji na sherehe.

19Akaweka walinzi kwenye milango ya nyumba ya Yawe kusudi mutu yeyote anayehesabiwa kuwa muchafu kwa njia moja au nyingine asiingie.

20Alitwaa majemadari wa jeshi, waheshimiwa, watawala wa watu, na wakaaji wote; nao wakamusindikiza mufalme kutoka nyumba ya Yawe, wakapitia katika mulango wa juu mpaka kwenye nyumba ya kifalme. Kisha wakamuikalisha mufalme kwenye kiti cha kifalme.

21Kwa hiyo wakaaji wote wakajaa na furaha; na muji wote ukakuwa mutulivu nyuma ya Atalia kuuawa kwa upanga.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help