Ezekieli 3 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Akaniambia: Wewe mwanadamu, kula unachopewa; kula kizingo hiki cha kitabu, kisha uende kusema na Waisraeli.

2Kwa hiyo nikafungua kinywa changu, naye akanikulisha kile kitabu.

3Halafu akaniambia hivi: Wewe mwanadamu, kula kizingo hiki ninachokupa, ujaze tumbo lako na kulishibisha. Basi, nikakikula, nacho kikakuwa kitamu ndani ya kinywa changu kama vile asali.

4Kisha akaniambia hivi: Wewe mwanadamu, uwaendee Waisraeli, uwaambie maneno yangu.

5Mimi sikutumi kwa taifa lenye luga ya kigeni na lenye usemi mugumu, lakini kwa Waisraeli.

6Sikutumi kwa mataifa mengi yenye luga ya kigeni na ngumu ambayo hauifahamu. Hakika ningelikutuma kwa watu kama hao, hakika wao wangekusikiliza.

7Lakini Waisraeli watakataa kukusikiliza, maana hawataki kunisikiliza mimi. Watu wote wa Israeli ni wenye kichwa nguvu na moyo mugumu.

8Nimekufanya kuwa mugumu, na kichwa chako kuwa nguvu kwa kupingana nao.

9Kama vile almasi inavyokuwa ngumu kuliko mawe mengine, ndivyo nilivyokufanya ukuwe na kichwa kigumu. Usiwaogope wala usitishwe na nyuso zao, maana hao ni watu waasi.

10Tena akaniambia hivi: Wewe mwanadamu, maneno yote nitakayokuambia uyaweke ndani ya moyo wako, na uyasikilize vizuri.

11Kisha uende kwa watu wako waliopelekwa katika uhamisho, uwaambie kwamba: “Yawe anasema hivi”, wakisikia au wakikataa kusikia.

12Kisha Roho akaninyanyua juu, nami nikasikia nyuma yangu sauti kama ya tetemeko kubwa ikisema: Utukufu wa Yawe usifiwe mbinguni.

13Vilevile nilisikia sauti ya mabawa ya vile viumbe yalipokuwa yanagusana, pamoja na sauti ya shindo la yale magurudumu kandokando yao.

14Basi, Roho akaninyanyua juu na kunipeleka mbali. Yawe alinijaza uwezo wake. Nami nikaenda nikiwa na uchungu na hasira katika roho yangu.

15Nikawafikia wale watu waliokuwa katika uhamisho, waliokuwa wakiishi karibu na muto Kebari huko Teli-Abibu. Nikakaa nao kwa muda wa siku saba nikishangaa sana.

Ezekieli anakuwa bubu kwa muda(Eze 33.1-9)

16Nyuma ya siku saba, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:

17Wewe mwanadamu, nimekuweka kuwa mulinzi wa Waisraeli. Utakuwa ukisikiliza maneno ninayokuambia na kwenda kuwatolea maonyo yangu.

18Nikimwambia mutu mwovu kwamba hakika atakufa, nawe haumwonyi au kumwambia aache mwenendo wake mubaya apate kuyaokoa maisha yake, basi, mutu huyo mwovu atakufa kwa uovu wake; lakini wewe utabeba lazima ya damu yake.

19Lakini, ukimwonya mutu huyo mwovu naye hauachi uovu wake au mwenendo wake mubaya, mutu huyo atakufa kwa ajili ya uovu wake, lakini wewe utakuwa umeyaokoa maisha yako.

20Tena, kama mutu wa haki akigeuka katika haki yake na kutenda uovu, nami nikimwekea kikwazo, mutu huyo atakufa. Kwa vile haukumwonya, atakufa kwa sababu ya zambi yake, nayo matendo yake ya haki hayatakumbukwa. Lakini wewe utabeba lazima ya damu yake.

21Lakini, ukimwonya mutu wa haki asitende zambi, naye akiacha kutenda zambi, hakika mutu huyo ataishi, kwa sababu amepokea maonyo yako, nawe utakuwa umeyaokoa maisha yako.

22Yawe akanijaza uwezo wake; naye akaniambia: Simama, uende katika bonde nami nitaongea nawe huko.

23Basi, nikasimama na kwenda katika bonde. Nikiwa huko nikauona utukufu wa Yawe ukiwa umesimama huko kama utukufu ule niliokuwa nimeuona karibu na muto Kebari; nami nikaanguka uso mpaka chini.

24Lakini roho ya Mungu aliniingia na kunisimamisha wima. Kisha Mungu akaongea nami, akaniambia: Kwenda ujifungie ndani ya nyumba yako.

25Ewe mwanadamu, utafungwa kwa kamba kusudi usiweze kutoka na kuwaendea watu.

26Nitaufanya ulimi wako ukuwe muzito nawe utakuwa bubu kusudi usiweze kuwakaripia kwa sababu ni waasi.

27Lakini wakati nitakaposema nawe nitakifungua kinywa chako, nawe utawaambia kwamba: “Yawe anasema hivi”. Atakayesikia, asikie; atakayekataa kusikia, akatae; maana hao ni watu waasi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help