1Siku tatu nyuma ya kufika kwake katika jimbo lile, Festo akaondoka Kaisaria na kwenda Yerusalema.
2Kule wakubwa wa makuhani na wakubwa wa Wayuda wakamushitaki Paulo mbele yake.
3Wakamusihi Festo awafanyie wema kwa kuwaletea Paulo Yerusalema, kwa maana walikuwa wakivizia kumwua katika njia.
4Festo akajibu: “Paulo analindwa katika kifungo kule Kaisaria, na mimi mwenyewe nitaenda kule sasa hivi.
5Basi wamoja kati ya wakubwa wenu waende pamoja nami Kaisaria nao wamushitaki kule ikiwa alifanya ubaya wowote.”
6Kisha kukaa pamoja nao muda wa siku nane au kumi, Festo akarudi Kaisaria. Kesho yake akaikaa ndani ya tribinali na kuamuru wamulete Paulo.
7Wakati Paulo alipofika, wale Wayuda waliotoka Yerusalema wakamuzunguka na kutoa mashitaki mengi mazito juu yake ambayo wao hawawezi kuhakikisha.
8Halafu Paulo akajitetea, akisema: “Mimi sikufanya kosa lolote juu ya Sheria ya Musa, juu ya hekalu, wala juu ya Mufalme wa Roma.”
9Festo aliyetaka kujipendekeza kwa Wayuda, akamwuliza Paulo: “Unataka niende kukusambishia maneno haya kule Yerusalema?”
10Paulo akajibu: “Mimi ninasimama mbele ya tribinali ya Mufalme wa Roma, na ni hapa ninapopaswa kusambishwa. Sikuwakosea Wayuda kosa lolote, kama vile wewe mwenyewe unavyojua vizuri.
11Kama mimi ni mukosaji au nimefanya kitendo kinachonipasa kuuawa, mimi sikatai kufa. Lakini kama hakuna ukweli wowote katika mashitaki yao juu yangu, hakuna mutu anayeweza kunitoa kwao. Ninaomba kusambishwa na Mufalme wa Roma.”
12Basi Festo alipokwisha kukata shauri pamoja na washauri wake, akajibu: “Unaomba kusambishwa na Mufalme wa Roma, basi utakwenda kwa Mufalme wa Roma.”
Liwali Festo anaomba shauri kwa mufalme Agripa13Kulipopita siku chache, mufalme Agripa na dada yake Berenike wakafika Kaisaria kumusalimia Festo.
14Kufuatana na vile walikaa kule siku nyingi, Festo akamwelezea mufalme maneno ya Paulo. Akamwambia: “Hapa kuna mutu mumoja aliyeachwa na Feliki katika kifungo.
15Wakati nilipokwenda Yerusalema, wakubwa wa makuhani na wazee wa Wayuda walimushitaki na kuniomba nimuhukumu.
16Nami nikawajibu kwamba si desturi ya Waroma kumutoa mutu yeyote aliyeshitakiwa mbele ya kusamba uso kwa uso na washitaki wake na kupata nafasi ya kujitetea juu ya jambo walilomushitakia.
17Basi walipofika hapa pamoja nami, sikupoteza wakati lakini kesho yake nikaikaa ndani ya tribinali na kuamuru wamulete mutu yule.
18Nao washitaki wake waliposimama, hawakumushitaki juu ya neno baya kama nilivyokuwa ninawazia.
19Walikuwa tu wakibishana naye juu ya dini yao wenyewe na juu ya mutu mumoja aliyeitwa Yesu; lakini Paulo alidai kwamba yuko muzima.
20Kwa ngambo yangu sikujua nifanye nini kwa kuchunguza ukweli wa mabishano hayo. Nikamwuliza Paulo kama anataka kwenda Yerusalema kusambishwa kule juu ya maneno yale.
21Lakini wakati Paulo alipoomba maneno yake yakatwe na Mufalme wa Roma, nikaamuru alindwe katika kifungo mpaka nitakapomutuma kwa Mufalme wa Roma.”
22Halafu Agripa akamwambia Festo: “Na mimi vilevile ningependa kumusikiliza mutu huyu peke yangu.”
Festo akajibu: “Utamusikiliza kesho.”
23Basi kesho yake Agripa pamoja na Berenike walifika katika shangwe kubwa na kuingia katika chumba cha mukutano, pamoja na wakubwa wa jeshi, na wakubwa wa muji. Festo akaamuru wamulete Paulo.
24Halafu Festo akasema: “Mufalme Agripa, na ninyi wote munaokuwa hapa pamoja nasi, munamwona mutu huyu Wayuda wote waliyemushitaki kwangu kule Yerusalema na hapa vilevile wakilalamika kwamba hastahili kuishi tena.
25Mimi niliona kwamba hakufanya kitendo chochote cha kustahili kufa. Lakini kwa sababu yeye mwenyewe aliomba maneno yake yakatwe na Mufalme wa Roma, nilikusudia kumutuma kwake.
26Mimi sina maneno kamili ya kumwandikia Mufalme wa Roma juu yake. Ndiyo maana nimemuleta mbele yenu na zaidi mbele yako, wewe mufalme Agripa, kusudi kisha kumwuliza, nipate maneno ya kuandika.
27Kwa sababu ninaona kwamba haina maana kumutuma mufungwa pasipo kueleza wazi mashitaki juu yake.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.