Yobu 11 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Kisha Zofari wa inchi ya Namati akamujibu Yobu:

2Wingi huu wa maneno uachwe tu bila kujibiwa?

Mutu wa maneno mengi anaonyesha kwamba hana kosa?

3Kupapayuka kwako kutanyamazisha watu?

Kama ukichekelea watu, hakuna atakayekupatisha haya?

4Wewe unasema: “Masemi yangu ni safi,

mimi sina kosa mbele ya Mungu.”

5Heri Mungu angefungua kinywa chake

na kutoa sauti yake kwa kukujibu!

6Angekuelezea siri za hekima,

maana yeye yuko na maarifa mengi.

Ujue kwamba Mungu hakuhesabu makosa yako yote.

7Unaweza kuvumbua siri za Mungu

na kujua ukomo wa Mungu Mwenye Uwezo?

8Ukubwa wake unapita mbingu;

wewe unaweza nini?

Kimo chake kinapita kuzimu;

wewe unaweza kujua nini?

9Ukubwa ule unapita urefu wa dunia,

unapita upana wa bahari.

10Kama Mungu akipita,

akimufunga mutu na kumuhukumu,

nani anayeweza kumuzuia?

11Mungu anajua watu wasiofaa;

anaona uovu vilevile bila magumu.

12Mupumbafu hawezi kuwa na maarifa.

Punda wa pori ni punda wa pori tu.

13Yobu, ukifanya moyo wako mukamilifu,

utainua mikono yako kwa kumwomba Mungu!

14Kama uovu uko katika mukono wako, uutupilie mbali.

Usikubali ubaya ukuwe katika nyumba yako.

15Halafu utainua uso wako bila kosa,

utakuwa imara bila kuwa na hofu.

16Utazisahau taabu zako zote;

utazikumbuka tu kama mafuriko yaliyopita.

17Maisha yako yataangaa kuliko jua la muchana kati,

giza lake litabadilika kuwa mapambazuko.

18Utakuwa na uhakika maana kuna tumaini;

utalindwa na kupumzika salama.

19Utalala bila kuogopeshwa na mutu;

watu wengi watakuomba musaada.

20Lakini waovu macho yao yatafifia,

njia zote za kutorokea zitawapotea;

tumaini lao la mwisho ni kukata roho!

Jibu la Yobu
Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help