1Yoasi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala. Alitawala kwa muda wa miaka makumi ine kule Yerusalema. Mama yake alikuwa Sibia kutoka Beri-Seba.
2Wakati wote kuhani Yoyada alipokuwa muzima, Yoasi alitenda mema mbele ya Yawe.
3Yoyada akamwoea wake wawili, nao wakamuzalia wana na wabinti.
4Nyuma ya hayo Yoasi akaamua kujenga nyumba ya Yawe.
5Basi, akawaita makuhani na Walawi na kuwaamuru: “Mwende katika miji ya Yuda, mukusanye feza kutoka kwa Waisraeli wote kwa kujenga upya nyumba ya Mungu wenu kila mwaka. Mufanye haraka.” Lakini Walawi hawakufanya haraka.
6Basi mufalme akamwita kiongozi Yoyada, akamwuliza: “Mbona haujaamurisha Walawi kukusanya kutoka kwa watu wa Yuda na Yerusalema, kodi ambayo Musa mutumishi wa Yawe aliagiza watu walipe kwa ajili ya Hema Takatifu la Yawe?” Ang. Kut 30.11-16
7Kwa sababu wana wa Atalia, yule mwanamuke mwovu walivunja nyumba ya Mungu na kuingia ndani; vilevile vyombo vitakatifu vya nyumba ya Yawe walivitumia katika ibada za Mabali.
8Basi mufalme akawaamuru, watengeneze sanduku la matoleo na kuliweka inje ya mulango wa nyumba ya Yawe.
9Kisha tangazo likatolewa kote katika Yuda na Yerusalema, kwamba watu wote wamuletee Yawe kodi ambayo Musa mutumishi wa Mungu, aliwaamuru Waisraeli walipokuwa katika jangwa.
10Wakubwa wote na watu wote wakafurahi wakaleta kodi yao wakaitumbukiza kwenye sanduku mpaka walipomaliza kufanya hivyo.
11Walawi walipopeleka sanduku hilo kwa wakubwa wa mufalme, nao walipoona kwamba kuna kiasi kikubwa cha feza ndani, katibu wa mufalme pamoja na musimamizi wa Kuhani Mukubwa, wakazitoa ndani ya sanduku, kisha wakalirudisha kwa nafasi yake. Waliendelea kufanya vile kila siku, wakakusanya feza nyingi.
12Mufalme na Yoyada walitoa feza zile na kuwapa wale waliosimamia kazi ya kujenga upya nyumba ya Yawe. Nao wakalipa wajengaji, waseremala kwa kutengeneza nyumba ya Yawe. Wakalipa vilevile wafuaji wa chuma na shaba kwa kujenga upya nyumba ya Yawe.
13Hivyo wafundi hao walishugulika na kazi hiyo kwa bidii, wakairudisha nyumba ya Yawe katika hali yake ya zamani, na kuiimarisha.
14Walipomaliza kutengeneza nyumba ya Yawe, wakamuletea mufalme na Yoyada zahabu na feza iliyobaki; halafu vyombo kwa ajili ya nyumba ya Yawe vilitengenezwa kwa feza hizo, vyombo hivyo vilikuwa vya kutumika katika kazi ya nyumba ya Yawe, matoleo ya sadaka za kuteketeza kwa moto na mabakuli ya kufukizia ubani, vilevile vyombo vya zahabu na vya feza. Watu waliendelea kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto katika nyumba ya Yawe wakati wote wa Yoyada.
Mashauri ya Yoyada yanakataliwa15Lakini Yoyada akazeeka na alipofikisha umri wa miaka mia moja na makumi tatu, akakufa.
16Wakamuzika katika muji wa Daudi, kwenye makaburi ya wafalme kwa kuonyesha heshima yao kwake kwa sababu alifanya mema katika Israeli na mbele ya Mungu na nyumba yake.
17Nyuma ya kifo cha Yoyada, wakubwa wa Yuda wakamwendea mufalme Yoasi wakainama uso mpaka chini mbele yake, wakamushawishi, naye akakubaliana nao.
18Basi, watu wakaacha kuabudu katika nyumba ya Yawe, Mungu wa babu zao, wakaanza kuabudu Maashera na sanamu. Kasirani ya Mungu ikawaka juu ya Yuda na Yerusalema kwa sababu ya kosa lile.
19Hata hivyo, akawatumia manabii kwa kuwaonya kusudi wamurudilie Yawe, lakini wao hawakuwasikiliza.
20Halafu Roho wa Mungu akamujaza Zakaria mwana wa kuhani Yoyada, naye akasimama mbele ya watu kwa pahali palipokuwa juu kidogo, akawaambia: “Yawe anauliza: Kwa nini mumevunja sheria zake? Sasa hamuwezi kufanikiwa! Kwa vile mumemwacha, naye vilevile amewaacha!” Ang. Mat 23.35; Lk 11.51
21Lakini wakamufanyia shauri baya; na kwa amri ya mufalme, wakamupiga mawe kwenye kiwanja cha nyumba ya Yawe.
22Mufalme Yoasi akasahau mema yote aliyotendewa na Yoyada, baba ya Zakaria, akamwua mwana wake. Alipokuwa karibu kufa, alisema: “Yawe uangalie mambo haya na kuyalipiza.”
Mwisho wa utawala wa Yoasi23Kwa mwisho wa mwaka, jeshi la Wasuria lilishambulia Yerusalema na Yuda. Wakawaua wakubwa wote, wakanyanganya vitu vingi na kuvituma kwa mufalme wa Damasiki.
24Ingawa jeshi la Suria lilikuwa dogo, Yawe alilipatia ushindi mbele ya jeshi kubwa la watu wa Yuda kwa sababu hao watu wa Yuda walikuwa wamemwacha Yawe, Mungu wa babu zao. Hivi, Wasuria wakatimiza azabu ya Mungu juu ya mufalme Yoasi.
25Waadui walipoondoka, wakamwacha akiwa ameumizwa vibaya sana, wakubwa wake wakamufanyia shauri baya, wakamwua juu ya kitanda chake, kwa kulipiza kisasi cha mauaji ya mwana wa kuhani Yoyada. Alizikwa katika muji wa Daudi, lakini si kwenye makaburi ya wafalme.
26Watu waliomufanyia shauri baya walikuwa ni Zabadi mwana wa mwanamuke Mwamoni jina lake Simeati, na Yozabadi mwana wa mwanamuke Mumoabu jina lake Simuriti.
27Habari za wana wake, za kujenga upya nyumba ya Yawe, na unabii wote juu yake, zimeandikwa katika maelezo ya kitabu cha Wafalme. Amazia mwana wake akatawala pahali pake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.