1Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mutume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, kwa kutangaza ahadi ya uzima tunaokuwa nao katika kuungana na Yesu Kristo.
2Ninakuandikia wewe Timoteo, mwana wangu mupendwa. Ninakutakia neema, rehema, na amani kutoka kwa Mungu Baba na kwa Bwana wetu Kristo Yesu.
Shukrani na maonyo3Ninamushukuru Mungu ambaye ninamutumikia kwa zamiri safi kama vile babu zangu walivyofanya, ninapokukumbuka siku zote katika maombi yangu usiku na muchana.
4Nikikumbuka machozi yako, ninatamani sana kukuona kusudi nipate kujazwa na furaha.
5Ninakumbuka vilevile imani yako isiyokuwa ya udanganyifu, imani ile tate muzaa mama yako Loisi na mama yako Euniki waliyokuwa nayo. Ninajua hakika kwamba wewe vilevile uko nayo.
6Kwa sababu hii ninakukumbusha uchochee zawadi ya Mungu uliyoipokea nilipoweka mikono juu yako.
7Kwa maana Mungu hakutupatia sisi Roho wa kuogopa, lakini Roho anayetupatia nguvu, upendo na kujizuiza.
8Basi, usisikie haya ya kutoa ushuhuda kwa ajili ya Bwana wetu, wala usisikie haya kwa sababu yangu mimi ninayekuwa katika kifungo kwa ajili yake. Lakini ushiriki nami katika mateso kwa ajili ya Habari Njema, kufuatana na uwezo unaopewa na Mungu.
9Yeye ndiye aliyetuokoa na kutuita kuwa watu wake, si kwa sababu ya matendo lakini ni kwa sababu ya mupango wake mwenyewe na neema yake aliyotupatia katika kuungana na Kristo Yesu mbele ya nyakati zote.
10Lakini neema hii imeonekana sasa kwa kuja kwa Mwokozi wetu Kristo Yesu. Yeye ameshinda nguvu za lufu na kwa njia ya Habari Njema ameonyesha wazi uzima wa milele.
11Kwa ajili ya Habari Njema hii, nimewekwa kuwa mujumbe, mutume na mwalimu,
12na kwa sababu hiyo ninapata mateso haya. Lakini sisikii haya kwa ajili ya ile. Maana ninajua ni nani yule niliyemwamini, nami ninahakikisha kwamba anaweza kuchunga kile alichonipa kwa kunilinda mpaka Siku ile ya kurudi kwake.
13Ushike maneno ya kweli niliyokufundisha, yapate kuwa mufano kwako. Ushikamane na imani na upendo unaokuwa nao kwa njia ya kuungana kwako na Kristo Yesu.
14Kwa nguvu za Roho Mutakatifu anayekaa ndani yetu, uchunge kile kitu kizuri ulichopewa kwa kulinda.
15Kama unavyojua wewe mwenyewe, watu wote wa jimbo la Azia wameniacha; kati yao kuna Figelo na Hermogene.
16Bwana awajalie mema sana watu wa jamaa ya Onesiforo, kwa maana amekuja mara nyingi kunifariji, wala hakusikia haya kwa kuniona niko katika kifungo.
17Wakati alipofika Roma, alinitafuta kwa bidii sana mpaka akaniona.
18Bwana amusikilie huruma kwa Siku ile! Unajua vizuri sana vilevile mambo yote aliyonitendea kule Efeso.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.