Mezali UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002
UTANGULIZIKitabu cha Mezali ni kimoja kati ya “vitabu vya hekima” katika Agano la Kale. Vitabu vingine vya namna hii ni Yobu na Muhubiri. Kitabu chenyewe kina mukusanyo wa mezali mbalimbali ambazo kwa jumla kusudi lake ni kuwafundisha watu maisha bora. Nyingi zinatajwa kuwa za mufalme Solomono ambaye alijulikana kama mwenye hekima mukubwa kabisa. Kitabu hiki kinaweza kugawanyika hivi:Sura 1-9: Utangulizi juu ya hekima. Katika sehemu hii tunaelezwa wazi kazi ya hekima. Hekima hapa inazungumuziwa sawa vile ni mutu.Sura 10-29: Hapa tuna mukusanyo wa mezali zinazotajwa kama za mufalme Solomono (10.1–22.16; 25.1–29.27), pamoja na nyingine ambazo zinatoka kwa wenye hekima wengine (22.17–24.34).Sura 30-33: Katika sehemu hii kuna visehemu vine tofauti, viwili vikitupasha juu ya mafikiri na maonyo ya wenye hekima wasiokuwa Wayuda (30.11-14 na 31.1-9).