Yobu 14 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Mutu anazaliwa na mwanamuke,

ana siku chache, na taabu nyingi.

2Anachanua kama maua, kisha ananyauka.

Anakimbia kama kivuli na kutoweka.

3Ee Mungu, kwa nini unajali hata kumwangalia

na kuanza kusamba naye?

4Nani anayeweza kutoa kitu kisafi kutoka kitu kichafu?

Hakuna anayeweza.

5Siku za kuishi za mwanadamu zimepimwa.

Ee Mungu, umepanga hesabu ya miezi yake;

hawezi kupita mupaka uliomwekea.

6Angalia pembeni basi, umwache,

kusudi apate kufurahia siku zake kama mutumishi wa mushahara.

7Muti ukikatwa, kuna tumaini la kuota,

unaweza kuchipuka tena.

8Japo mizizi yake itazeeka katika udongo,

na shina lake kukufia ndani ya udongo,

9lakini kwa harufu tu ya maji utachipuka,

utatoa matawi kama chipukizi.

10Lakini mutu anakufa na ule ndio mwisho wake.

Akisha kutoa roho, anabakiliwa na nini tena?

11Kama vile maji yanavyokauka katika ziwa,

na muto unavyokoma kutiririka,

12ndivyo mutu anavyokufa, wala haamuki tena.

Hataamuka tena wala kusisimuka,

hata pale mbingu zitakapotoweka.

13Heri ungenificha katika kuzimu,

ungenificha mpaka kasirani yako itulie,

nawe ungenipimia muda kwa kunikumbuka tena.

14Mutu akikufa anaweza kuishi tena?

Siku zangu zote za kazi ningekungoja

mpaka wakati wa kufunguliwa ufike.

15Halafu ungeniita, nami ningeitika,

wakati ungetaka kuniona mimi kiumbe chako.

16Kwa hiyo ungeweza kuhesabu hatua zangu,

ungeacha kuchunguza zambi zangu.

17Makosa yangu yangefungiwa katika mufuko,

nawe ungefunika uovu wangu.

18Lakini milima inaanguka

nayo mawe yanaongoka pahali pake.

19Mitiririko wa maji inakulakula mawe,

mvua kubwa inaleta mumomonyoko wa udongo.

Ndivyo nawe unavyoharibu tumaini la mwanadamu.

20Wewe unamwangusha mwanadamu, naye anatoweka milele;

unaubadilisha uso wake na kumutupilia mbali.

21Watoto wake wakiheshimika, yeye hana habari.

Wakizarauliwa, yeye haoni kabisa.

22Anasikia tu maumivu ya mwili wake,

na kuomboleza tu hali yake mbaya.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help