1Kutoka jangwa la Sini, Waisraeli wote pamoja wakasafiri hatua kwa hatua kama vile Yawe alivyoamuru. Watu wakapiga kambi kule Refidimu. Lakini kule hakukukuwa maji ya kunywa.
2Kwa hiyo watu wakamunungunikia Musa wakisema: “Utupatie maji ya kunywa.”
Musa akawauliza: “Mbona munaninungunikia? Mbona munamujaribu Yawe?”
3Lakini wote walikuwa na kiu, wakamunungunikia Musa wakisema: “Kwa nini ulitutoa kule Misri utuue kwa kiu, sisi wote na watoto wetu na mifugo yetu?”
4Basi, Musa akamulilia Yawe akisema: “Nitawafanyia nini watu hawa? Wako karibu kunipiga mawe!”
5Yawe akamwambia Musa: “Pita mbele ya watu hawa ukipeleka wazee wao wamoja. Twaa vilevile katika mukono wako ile fimbo uliyoipiga nayo muto Nili.
6Angalia mimi nitasimama mbele yako juu ya jiwe la mulima wa Horebu, nawe utapiga lile jiwe na maji yatabubujika kutoka mule kusudi watu wote wapate kunywa.” Basi, Musa akafanya hivyo mbele ya wazee wa Waisraeli.
7Pahali pale Musa akapaita “Masa” na “Meriba”, ni kusema “Ujaribu” na “Magombano”, kwa sababu Waisraeli walimugombanisha na kumujaribu Yawe wakisema: “Kweli Yawe yuko pamoja nasi?”
8Waamaleki walikuja na kupigana na Waisraeli kule Refidimu.
9Musa akamwambia Yoshua: “Chagua wanaume uende upigane na Waamaleki. Kesho nitasimama juu ya kilele cha kilima, nikishika katika mukono wangu ile fimbo ya Mungu.”
10Basi, Yoshua akafanya kama vile Musa alivyosema, akaenda kupigana na Waamaleki. Musa, Haruni na Huri wakapanda juu ya kilele cha kilima.
11Ikakuwa wakati wote Musa alipoinua mukono wake juu, Waisraeli walishinda na alipouteremusha, Waamaleki walishinda.
12Lakini kisha muda, mikono ya Musa ikachoka. Kwa hiyo Haruni na Huri wakatwaa jiwe wakaliweka karibu na Musa naye akaikaa. Kisha wakaishika na kuiinua mikono yake. Mumoja akauinua mukono wa kuume na mwingine mukono wa kushoto. Hivyo mikono ya Musa ikabaki imara ikiwa imeinuliwa juu mpaka jua lilipotua.
13Yoshua akawakatakata Waamaleki.
14Kisha Yawe akamwambia Musa: “Uandike jambo hili katika kitabu, likuwe ukumbusho. Tena umwambie Yoshua kwamba nitawafuta kabisa Waamaleki katika dunia.” Ang. Kumb 25.17-19; 1 Sam 15.2-9
15Musa akajenga mazabahu na kuita mazabahu hiyo “Yawe ni Bendera Yangu”,
16akisema: “Muinue juu bendera ya Yawe! Yawe atapigana na Waamaleki kizazi kwa kizazi!”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.