1Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mutume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tunayemutumainia.
2Ninakuandikia wewe Timoteo mwana wangu wa kweli katika imani. Ninakutakia neema na rehema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.
Kuepuka mafundisho ya uongo3Ukae kule Efeso sawa vile nilivyokusihi wakati nilipokwenda Makedonia. Na kule uwazuize wale watu wanaofundisha mafundisho ya uongo.
4Uwaambie wasishikamane na hadisi za uongo, pamoja na mambo yasiyokuwa na mwisho ya wababu. Hayo yote yanaleta mabishano, wala hayafai kitu kwa kutimiza mupango wa Mungu wa wokovu, unaojulikana kwa njia ya imani.
5Shabaha ya agizo hilo ni kusudi kuwe upendo unaotokana na moyo safi na zamiri nzuri na imani ya kweli.
6Watu wamoja wamekosa kuwa na tabia hiyo hata wamefuata maneno ya ovyo ovyo.
7Wanataka kuwa walimu wa Sheria ya Musa, lakini hawaelewi wao wenyewe maneno wanayosema wala maneno wanayohakikisha.
8Tunajua kwamba Sheria ni nzuri, kama ikitumiwa kwa njia ya haki.
9Vilevile ni sherti kujua kwamba Sheria haikuwekwa kwa ajili ya wenye haki, lakini kwa ajili ya watenda mabaya, waasi, watu wasiomuheshimu Mungu, wenye zambi, nao wenye kuchafua vitu vitakatifu na kukufuru, na kwa ajili ya wale wanaowaua wababa zao au wamama zao, na wauaji wowote.
10Sheria imewekwa kwa ajili ya waasherati, wanaume wanaozini wao kwa wao, wenye kuuzisha watu, wasema uongo, wale wanaofanya viapo vya uongo na kwa ajili ya wote wanaofanya matendo yanayokuwa umbalimbali na mafundisho ya kweli.
11Mafundisho haya yanalingana na Habari Njema ya utukufu wa Mungu mwenye baraka, ambayo nilipewa nipate kuihuburi.
Kushukuru wema wa Mungu12Ninamushukuru Bwana wetu Kristo Yesu aliyenitia nguvu, kwa sababu alinihesabu kuwa mwaminifu hata akaniweka kwa kazi yake.
13Ingawa zamani nilikuwa mwenye kumutukana, mwenye kumutesa na kumutendea kwa ukali, lakini amenihurumia, kwa sababu yote niliyofanya, niliyafanya kwa upumbafu kwa maana sikukuwa bado na imani.
14Bwana wetu amenijalia neema kwa uwingi, amenipa imani na upendo tunaokuwa nao katika kuungana kwetu na Kristo Yesu.
15Neno hili ni la kuaminiwa nalo linastahili kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja katika dunia kwa kuokoa wenye zambi. Na mimi ni wa kwanza mwenye zambi kati yao,
16lakini kwa sababu hiyo Mungu amenihurumia. Alifanya vile kusudi kwa njia yangu mimi ninayekuwa mutenda zambi wa kwanza, Yesu Kristo apate kuonyesha uvumilivu wake. Na hivi mimi nipate kuwa mufano kwa wote watakaoamini nyuma na kupata uzima wa milele.
17Kwa Mufalme wa milele, asiyeweza kufa, asiyeonekana, Mungu peke yake, ikuwe heshima na utukufu milele na milele! Amina.
18Timoteo mwana wangu, ninakupa agizo hili kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa zamani juu yako. Maneno hayo ndiyo yatakayokuwezesha kupiga vita nzuri,
19ukichunga imani yako na kuwa na zamiri safi. Watu wamoja wamekataa kuwa na zamiri hata wamepoteza imani yao.
20Kati yao kuna Himeneo na Alesanduro, ambao nimemwachia Shetani kusudi wasimutukane Mungu tena.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.