1Basi, sisi tunaotumika pamoja na Mungu, tunawasihi musipoteze bure neema muliyopokea kwake.
2Kwa maana Mungu anasema hivi katika Maandiko Matakatifu:
“Kwa wakati uliofaa, nilijibu maombi yako.
Kwa siku ya wokovu, nilikusaidia.”
Basi sasa, huu ndio wakati unaofaa, sasa leo ni siku ya wokovu.
3Sisi hatutaki kumukwaza mutu yeyote katika jambo lolote kusudi kazi yetu isizarauliwe.
4Lakini tunaonyesha katika mambo yote kwamba sisi ni watumishi wa Mungu: tumedumu sana katika mateso, katika ukosefu na katika taabu.
5Tumepigwa, tumetiwa ndani ya kifungo, wamefanya fujo juu yetu, tumefanya kazi ngumu, tumekoseshwa usingizi na kukaa bila kula.
6Tunaonyesha kwamba sisi ni watumishi wa Mungu kwa njia ya usafi wa moyo wetu, ya ufahamu, ya uvumilivu, ya wema wetu, ya Roho Mutakatifu, ya upendo wetu wa kweli,
7ya ujumbe wa neno la kweli, na ya uwezo wa Mungu. Tunatumia kama vile silaha mambo ya haki kwa kushambulia na kujikinga.
8Tunaheshimiwa na kuzarauliwa, tunatukanwa na kusifiwa. Tunahesabiwa kama wenye kusema uongo, ingawa sisi tunasema ukweli,
9kama watu wasiojulikana ingawa tunajulikana vizuri, kama wanaokufa ingawa sisi ni wazima. Tunaazibiwa lakini hatuuawi,
10tunahuzunishwa lakini tunafurahi siku zote. Tunaonekana kama wamasikini lakini tunatajirisha watu wengi, hatuna kitu, lakini tunakuwa na vitu vyote.
11Ee ninyi Wakorinto! Tumesema nanyi waziwazi na tumewafungulia kabisa moyo wetu.
12Sisi hatukuwafungia mioyo yetu, lakini ni ninyi ndio muliotufungia moyo wenu.
13Sasa ninasema nanyi kama vile watoto wangu: kwa ngambo yenu mutufungulie nasi moyo wenu vilevile.
Kujitenga na ubaya14Musishirikiane pamoja na watu wasioamini. Kwa maana kuna ushirika gani kati ya haki na uovu? Kuna mapatano gani kati ya mwangaza na giza?
15Kuna masikilizano gani kati ya Kristo na Shetani? Au mutu anayeamini yuko na ushirika gani na mutu asiyeamini?
16Kuna ulinganisho gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi ni hekalu la Mungu Mwenye Uzima kama vile yeye mwenyewe alivyosema:
“Nitakaa na kuishi pamoja nao,
nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
17Kwa sababu hiyo Bwana anasema:
“Mutoke kati yao, mujitenge nao.
Musiguse kitu chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu,
nami nitawapokea.
18Nitakuwa Baba yenu
nanyi mutakuwa wana na wabinti wangu.
Ni mimi Bwana Mwenye Uwezo ninayesema.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.