1Kwa mukubwa wa waimbaji: Zaburi ya Wakora.
2Ee Yawe,
umependelea inchi yako;
umerudishia wazao wa Yakobo hali nzuri.
3Umewasamehe watu wako kosa lao;
umefuta zambi zao zote.
4Umezuia kasirani yako yote;
umeacha hasira yako kali.
5Utustareheshe tena, ee Mungu mwokozi wetu;
uondoe chuki unayokuwa nayo juu yetu.
6Utatukasirikia hata milele?
Utadumisha kasirani yako kwa vizazi vyote?
7Hautatujalia tena maisha mapya,
kusudi watu wako wafurahi kwa sababu yako?
8Utuonyeshe wema wako, ee Yawe,
utujalie wokovu wako.
9Ninasikiliza yale Yawe anayosema,
maana anaahidi kuwapa watu wake amani,
watu wake mwenyewe wasiporudilia upumbafu wao.
10Hakika yeye ni tayari kuwaokoa wanaomuheshimu,
na utukufu wake utadumu katika inchi yetu.
11Wema na uaminifu vitakutana;
haki na amani vitashikamana.
12Uaminifu utachipuka katika inchi;
haki utashuka toka mbinguni.
13Kweli, Yawe atatuletea baraka,
na inchi yetu itatoa mazao yake mengi.
14Haki itamutangulia Mungu
na kumutayarishia njia yake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.