1Yawe alimwambia Musa:
2Uwaambie watu wa Israeli hivi: Kama mutu akitenda zambi bila kukusudia, akifanya kitu kilichokatazwa na amri ya Yawe, atafanya hivi:
3Ikiwa kuhani ambaye amepakwa mafuta ndiye aliyetenda zambi hata akawatia watu katika kosa, basi huyo atamutolea Yawe ngombe dume muchanga asiyekuwa na kilema akuwe sadaka kwa ajili ya zambi.
4Ataleta huyo ngombe dume muchanga kwenye mulango wa hema la mukutano, mbele ya Yawe. Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha ngombe dume huyo na kumuchinja mbele ya Yawe.
5Huyo kuhani aliyepakwa mafuta atatwaa sehemu ya damu na kuingia nayo ndani ya hema la mukutano.
6Atachovya kidole chake katika damu hiyo na kuinyunyiza mara saba mbele ya Yawe upande wa mbele wa pazia la Pahali Patakatifu.
7Kuhani atatwaa sehemu ya damu na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kufukizia ubani wenye harufu nzuri, mbele ya Yawe katika hema la mukutano. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka inayokuwa karibu na mulango wa hema la mukutano.
8Kisha ataondoa mafuta yote ya ngombe huyo: mafuta yanayofunika matumbotumbo,
9figo mbili na mafuta yanayokuwa juu yake na yale yanayokuwa kwenye kiuno na yale yanayoshikamana na figo na maini.
10Hizi ni sehemu zilezile zinazoondolewa kwa nyama wa sadaka ya amani. Kuhani ataziteketeza juu ya mazabahu ya kuteketezea sadaka.
11Lakini ngozi ya huyo ngombe, nyama, kichwa, miguu, matumbotumbo na mavi yake,
12ni kusema ngombe muzima aliyebakia atamupeleka na kumuteketeza inje ya kambi pahali safi ambapo majivu yanatupwa, naye atamuchoma kwa moto juu ya kuni. Atachomwa kwa moto pale pahali pa kumwangia majivu.
13Ikiwa Waisraeli wote pamoja wametenda zambi bila kukusudia kwa kufanya kitu kilichokatazwa na amri ya Yawe,
14mara tu zambi hiyo itakapojulikana, watatoa ngombe dume muchanga akuwe sadaka kwa ajili ya zambi. Watamuleta kwenye hema la mukutano.
15Wazee wao wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo ngombe dume, kisha atachinjwa mbele ya Yawe.
16Yule kuhani aliyechaguliwa kwa kupakwa mafuta ataleta sehemu ya damu ya huyo ngombe dume ndani ya hema la mukutano.
17Atachovya kidole chake katika hiyo damu na kuinyunyiza mbele ya pazia mara saba, mbele ya Yawe.
18Kisha, sehemu ya damu atazipakaa kwenye pembe za mazabahu inayokuwa katika hema la mukutano mbele ya Yawe. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka inayokuwa karibu na mulango wa hema la mukutano.
19Mafuta yote ya nyama huyo atayatwaa na kuyateketeza kwenye mazabahu.
20Kwa hiyo atamufanya ngombe dume huyu kama alivyomufanya yule mwingine wa sadaka kwa ajili ya zambi. Basi, huyo kuhani atawafanyia watu ibada hiyo ya upatanisho kwa ajili ya zambi, nao watasamehewa.
21Kisha atamutwaa ngombe dume huyu na kumupeleka inje ya kambi na kumuteketeza kwa moto kama vile alivyofanya yule mwingine. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi ya jamii.
22Ikiwa mutawala ametenda zambi bila kukusudia kwa kufanya kitu kilichokatazwa na amri ya Yawe, Mungu wake, na hivyo akakuwa na kosa,
23mara tu akijulishwa zambi hiyo aliyotenda, ataleta sadaka yake ya beberu asiyekuwa na kilema.
24Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha beberu na kumuchinjia pahali wanapochinjia sadaka za kuteketezwa mbele ya Yawe. Hiyo ni sadaka kwa ajili ya zambi.
25Kuhani atachovya kidole chake katika damu ya sadaka kwa ajili ya zambi na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kuteketezea sadaka. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka.
26Mafuta yote ya beberu huyo atayateketeza juu ya mazabahu, kama vile anavyofanya na mafuta ya nyama wa sadaka ya amani. Kwa hiyo kuhani atamufanyia mutawala ibada hiyo ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake, naye atasamehewa.
27Kama mutu wa kawaida ametenda zambi bila kukusudia, kwa kufanya kitu kilichokatazwa na amri ya Yawe na hivyo akakuwa na kosa, Ang. Hes 15.27-28
28mara tu atakapojulishwa kwamba ametenda zambi, ataleta sadaka ya mbuzi dike asiyekuwa na kilema kwa ajili ya zambi aliyotenda.
29Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha mbuzi huyo wa sadaka ya kuondoa zambi, na kumuchinjia pahali wanapochinjia nyama wa sadaka za kuteketezwa.
30Kuhani atachovya kidole chake katika damu ya sadaka ya kuondoa zambi na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kuteketezea sadaka. Damu iliyobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu.
31Mafuta yote ya mbuzi huyo atayaondoa kama vile anavyoondoa mafuta ya nyama wa sadaka ya amani, naye kuhani atayateketeza juu ya mazabahu, na harufu yake nzuri itamupendeza Yawe. Basi, kuhani atamufanyia yule mutu hiyo ibada ya upatanisho, naye atasamehewa.
32Ikiwa mutu yule ataleta mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya zambi, basi, ataleta mwana-kondoo dike asiyekuwa na kilema.
33Ataweka mukono wake juu ya kichwa cha mwana-kondoo huyo wa sadaka kwa ajili ya zambi na kumuchinjia pahali pale wanapochinjia nyama wa sadaka za kuteketezwa.
34Kisha kuhani atachovya kidole chake katika damu ya sadaka kwa ajili ya zambi na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kuteketezea sadaka. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu.
35Kisha ataondoa mafuta yote kama vile anavyoondoa mafuta ya mwana-kondoo wa sadaka ya amani na kuhani atayateketeza juu ya mazabahu, pamoja na sadaka zinazotolewa kwa Yawe kwa moto. Kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa ajili ya zambi yake, naye atasamehewa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.