Waefeso 4 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mwili mumoja

1Kwa hivi basi, mimi ninayekuwa mufungwa kwa sababu ninamutumikia Bwana, ninawasihi muishi sawa inavyostahili kufuatana na mwito Mungu aliowatolea.

2Mukuwe wanyenyekevu kabisa, wapole na wavumilivu. Muvumiliane ninyi kwa ninyi kwa upendo.

3Mujikaze sana kuchunga umoja wa Roho, kwa amani inayowaunganisha.

4Kuna mwili mumoja na Roho mumoja, vilevile kuna tumaini moja la mwito muliotolewa na Mungu.

5Kuna Bwana mumoja, imani moja, ubatizo mumoja;

6Mungu mumoja, Baba ya watu wote, anayekuwa juu ya wote, anayetumika kwa njia ya wote, na anayekaa ndani ya wote.

7Lakini kila mutu kati yetu alipokea neema kadiri ya kipimo alichojaliwa na Kristo.

8Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema:

“Alipopanda juu,

alikamata wafungwa,

aliwapatia watu zawadi.”

9Basi, neno hili “alipanda juu,” lina maana gani? Maana yake ni kusema kwamba alishuka kwanza mpaka chini katika dunia.

10Yule aliyeshuka ndiye yule yule aliyepanda juu sana kupita mbingu zote kusudi akamilike katika ulimwengu wote.

11Ni yeye ndiye aliwapatia watu zawadi za kipekee. Amewaweka wamoja kuwa mitume, wengine kuwa manabii, wengine kuwa watangazaji wa Habari Njema, wengine kuwa wachungaji na walimu.

12Yeye amefanya vile kwa kuwatayarisha watu wa Mungu kwa kazi ya utumishi kusudi mwili wa Kristo upate kujengwa.

13Hivi, sisi wote tutafikia umoja wa imani yetu na wa kumujua kabisa Mwana wa Mungu; tutapata kukomaa na kufikia kipimo cha utimilifu wa Kristo.

14Basi, hatutakuwa tena kama watoto, tukipeperushwa na kuvutwa na mafundisho ya kila aina yanayoletwa na watu wanaodanganya wengine na kuwapotosha kwa mayele yao.

15Lakini tukitangaza ukweli kwa upendo, tutakomaa katika mambo yote na kufikia kuwa kama Kristo, ambaye ni kichwa.

16Kwa uongozi wake, viungo vyote vya mwili vinashikamana kabisa, nao mwili wote muzima unashikamana vizuri kwa nguvu ya maunganio yake. Halafu, kila kiungo kinapotumika kama kinavyopaswa, mwili wote unakomaa na kujijenga katika upendo.

17Basi, kwa jina la Bwana ninawaonya hivi: musiishi tena kama watu wa mataifa mengine, wanaofuata mawazo yao ya bure

18na wenye mafikiri yaliyotiwa katika giza. Watu hawa hawashiriki katika uzima ule unaoletwa na Mungu, kwa sababu wao ni wapumbafu na wenye mioyo migumu.

19Hawasikii tena haya hata kidogo nao wamejitoa katika mambo ya ovyo na kufanya bila kujizuiza mambo yote mabaya.

20Lakini ninyi hamukujifunza vile juu ya Kristo!

21Hakika mumesikia habari zake, nanyi mukiwa waamini mumefundishwa kufuatana na ukweli unaokuwa ndani ya Kristo.

22Basi munapaswa kutupilia mbali ile hali yenu ya zamani, ule utu wenu wa zamani unaopotoka kufuatana na tamaa zake za udanganyifu.

23Inafaa mufanywe upya katika roho zenu na katika nia zenu.

24Mukuwe na hali mupya, inayoumbwa kwa mufano wa Mungu na inayoonekana katika maisha ya haki na utakatifu wa kweli.

25Kwa hivi, muache uongo! Kila mumoja aseme ukweli kwa mwenzake, kwa maana sisi wote ni viungo vya mwili mumoja.

26Kama mukikasirika, musianguke katika zambi, kasirani yenu isidumu muchana kutwa,

27wala musimufungulie Shetani mulango.

28Yule aliyekuwa akiiba, asiibe tena, lakini ajikaze kufanya kazi peke yake kwa usawa kusudi apate kuwasaidia wakosefu.

29Musiseme neno lolote baya, lakini kama ni lazima museme tu maneno mazuri na ambayo yanasaidia kuwajenga wengine na yanayoleta neema kwa wale wanaoyasikia.

30Musihuzunishe Roho Mutakatifu wa Mungu; kwa maana Roho ni kitambulisho kilichowekwa juu yenu kwa kuhakikisha kwamba ninyi ni watu wake mpaka siku Mungu atakapowakomboa.

31Mutupilie mbali nanyi nia zote za uadui, chuki, kasirani, fujo na masingizio. Mutupilie mbali ubaya wa kila namna!

32Lakini mutendeane wema ninyi kwa ninyi; musameheane kama Mungu alivyowasamehe ninyi kwa njia ya Kristo.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help