1Nebukadneza mufalme wa Babeli akaishambulia inchi ya Yuda. Yoyakimu akamutumikia kwa miaka mitatu halafu akaacha kumutii, akamwasi.
2Basi, Yawe akamupelekea makundi ya Wababeli, Waaramu, Wamoabu na Waamoni washambulie inchi ya Yuda na kuiharibu, kulingana na neno la Yawe alilolisema kwa njia ya watumishi wake manabii.
3Hakika mambo haya yakaitokea inchi ya Yuda kwa amri ya Yawe, kwa kuwahamisha kutoka mbele yake, kwa sababu ya zambi za mufalme Manase na yote aliyoyatenda,
4na kwa sababu ya damu isiyokuwa na kosa aliyoimwanga. Yawe hakumusamehe makosa hayo.
5Basi mambo mengine ya Yoyakimu na yote aliyofanya yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.
6Yoyakimu akakufa, na mwana wake Yoyakini akatawala kwa pahali pake.
7Mufalme wa Misri hakutoka tena katika inchi yake, kwa sababu mufalme wa Babeli alinyanganya inchi yote iliyokuwa mali ya Misri pale zamani, tangia kwenye kijito cha Misri mpaka kwenye muto Furati.
Mufalme Yoyakini wa Yuda(2 Sik 36.9-10)8Yoyakini alikuwa na umri wa miaka kumi na minane alipoanza kutawala. Alitawala akiwa Yerusalema kwa muda wa miezi mitatu. Mama yake aliitwa Nehusta, binti ya Elnatani, mukaaji wa Yerusalema.
9Alitenda maovu mbele ya Yawe kama vile baba yake alivyofanya.
10Wakati ule waaskari wa Nebukadneza mufalme wa Babeli wakashambulia Yerusalema na kuuzunguka.
11Wakati waaskari walipokuwa wanauzunguka muji, Nebukadneza mwenyewe alifika Yerusalema,
12na Yoyakini mufalme wa Yuda alijitoa kwa mufalme wa Babeli, yeye mwenyewe pamoja na mama yake, watumishi wake, wakubwa na majemadari wake. Mufalme wa Babeli aliwapeleka kama wafungwa katika mwaka wa nane wa kutawala kwake.
13Tena kama vile Yawe alivyosema, Nebukadneza alitwaa mali yote iliyokuwa ndani ya nyumba ya Yawe, na ndani ya nyumba ya kifalme. Akakatakata vyombo vyote vya zahabu ambavyo Solomono mufalme wa Israeli alitengeneza. Vyombo hivyo vilikuwa ndani ya hekalu la Yawe.
14Alitwaa watu wote wa Yerusalemu: wakubwa wote, watu wote waliokuwa mashujaa, wafungwa elfu kumi, na wafundi wote na wafuaji wa vyuma. Hakuna aliyebaki isipokuwa wale waliokuwa wamasikini kabisa katika inchi.
15Alimupeleka Yoyakini mpaka Babeli pamoja na mama ya mufalme, wake za mufalme, wakubwa wa waaskari wake, na wakubwa wa inchi wote. Hao aliwatoa Yerusalema. Akawapeleka katika uhamisho kule Babeli.
16Nebukadneza alipeleka watu mashujaa wa Yuda, jumla yao watu elfu saba pamoja na wafundi hodari na wafuaji wa vyuma elfu moja, wote hawa wakiwa watu wenye nguvu na wa kuweza kupigana katika vita.
17Nebukadneza akamuweka Matania, baba mudogo ya Yoyakini, kuwa mufalme kwa pahali pake, akalibadilisha jina lake kuwa Zedekia.
Mufalme zedekia wa Yuda(2 Sik 36.11-12; Yer 52.1-3a)18Zedekia alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mumoja alipoanza kutawala, alitawala kwa muda wa miaka kumi na mumoja akiwa kule Yerusalema. Mama yake aliitwa Hamutali binti wa Yeremia, mukaaji wa muji wa Libuna.
19Alitenda maovu mbele ya Yawe. Alifuata yote Yoyakimu aliyofanya.
20Yawe aliwakasirikia sana watu wa Yerusalema na Yuda, hata akawafukuza mbali naye. Zedekia alimwasi mufalme wa Babeli.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.