1Mupige baragumu!
Adui anakuja kama tai
kuishambulia nyumba ya Yawe,
kwa sababu wamelivunja agano langu
na kuiasi sheria yangu.
2Waisraeli wananililia wakisema:
Mungu wetu, sisi tunakujua.
3Lakini Waisraeli wametupilia mambo mazuri.
Kwa hiyo, sasa waadui watawafuatilia.
4Walijiwekea wafalme bila ruhusa yangu,
walijichagulia wakubwa ambao sikuwatambua.
Wamejitengenezea miungu ya feza na zahabu,
jambo ambalo litawaangamiza.
5Enyi watu wa Samaria, ninaichukia sanamu yenu ya mwana-ngombe.
Hasira yangu inawaka juu yenu.
Mutaendelea kuwa na makosa mpaka wakati gani?
6Ile sanamu inatoka Israeli,
ni fundi ndiye aliyeitengeneza.
Yenyewe si Mungu hata kidogo.
Kweli! Sanamu ya mwana-ngombe ya Samaria itavunjwavunjwa!
7Wanapanda upepo, watavuna zoruba!
Mimea yao ya ngano inayokuwa katika mashamba
haitatoa ngano yoyote.
Na hata kama ikizaa,
mazao yake yatakuliwa na wageni.
8Waisraeli wamemezwa,
wanakuwa kati ya mataifa mengine,
kama chombo kisichokuwa na faida yoyote.
9Wamekwenda kuomba musaada Asuria.
Efuraimu ni punda wa pori anayetangatanga peke yake;
Efuraimu amejilipia wapenzi wake.
10Wametafuta wapenzi kati ya watu wa mataifa,
lakini mimi nitawakusanya.
Na hapo watasikia uzito wa muzigo
wa mufalme wa wakubwa.
11Watu wa Efuraimu wamejijengea mazabahu nyingi,
na mazabahu hizo zimewazidishia zambi.
12Hata kama ningewaandikia sheria zangu mara nyingi,
wao wangeziona kuwa kitu cha kigeni tu.
13Wanapenda kutoa sadaka za nyama,
kwa kusudi la kula nyama yake;
lakini mimi Yawe sipendezwi hata kidogo.
Mimi ninayakumbuka makosa yao;
nitawaazibu kwa ajili ya zambi zao;
nitawarudisha katika utumwa kule Misri.
14Waisraeli wamemusahau Muumba wao,
wakajijengea nyumba kubwa;
watu wa Yuda wamejiongezea miji yenye kuzungukwa na kuta,
lakini mimi nitatuma moto katika miji hiyo,
na kuziteketeza kuta zao.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.