Zaburi 21 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Shukrani kwa ajili ya ushindi

1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.

2Ee Yawe,

mufalme anashangilia kwa nguvu yako,

anafurahi sana kwa musaada uliomupa.

3Umemutimizia mapenzi ya moyo wake;

wala haukumukatalia ombi lake.

4Umemufikia, ukamupatia baraka nzurinzuri;

umemuvalisha taji ya zahabu safi juu ya kichwa chake.

5Alikuomba maisha, nawe ukamupatia;

ulimupatia siku nyingi milele na milele.

6Kwa musaada wako, amepata utukufu sana;

wewe umemujalia sifa na heshima.

7Unamujalia baraka zako siku zote;

unamufurahisha kwa sababu uko pamoja naye.

8Mufalme anamutumainia Yawe;

kwa wema wa Mungu Mukubwa atakuwa salama.

9Mukono wako, ewe mufalme, utawakamata waadui zako wote;

mukono wako wa nguvu utawakamata wanaokuchukia.

10Utakapotokea utawaangamiza kama kwa moto wa furu.

Yawe atawamaliza kwa hasira yake,

moto utawateketeza kabisa.

11Utawaangamiza wazao wao watoweke katika dunia;

watoto wao hawatabaki kati ya wanadamu.

12Hata kama wakifanya shauri baya juu yako,

kama wakikamata mipango ya udanganyifu,

hawataweza kitu hata kidogo.

13Kwa maana wewe utapiga mishale mbele yao,

utawakimbiza mbio.

14Utukuzwe, ee Yawe, kwa sababu ya nguvu yako!

Tutaimba na kusifu kwa ajili ya uwezo wako.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help