1Siku ya Sabato ilipokwisha kupita, kesho yake siku ya kwanza ya juma, kwa wakati wa mapambazuko, Maria wa Magdala na Maria mwingine wakaenda kuangalia kaburi.
2Kwa rafla kukatokea tetemeko la inchi, kwa maana malaika wa Bwana alishuka toka mbinguni, akasukuma lile jiwe lililofunga kaburi pembeni na kuikaa juu yake.
3Yeye aliangaa kama umeme na nguo yake ilikuwa nyeupe sana.
4Halafu wale walinzi wa kaburi wakaogopa sana na kutetemeka, hata wakakuwa kama wamekufa.
5Yule malaika akawaambia wale wanawake: “Musiogope, kwa maana ninajua ya kama munamutafuta Yesu aliyetundikwa juu ya musalaba.
6Yeye hayuko hapa: amefufuka sawa alivyosema. Mukuje, muone pahali walipolalisha maiti yake.
7Muende upesi kuwaambia wanafunzi wake kwamba amefufuka, naye anawatangulia Galilaya, ni kule watakapomwona. Basi, nimekwisha kuwaambia ninyi.”
8Basi wale wanawake wakaondoka upesi kutoka kwenye kaburi, wakijazwa na woga na furaha kubwa vilevile. Wakakimbia kwenda kuwapasha wanafunzi wake habari ile.
9Mara moja Yesu akakutana na wale wanawake, akawasalimia. Wakajongea karibu naye, wakamushika miguu na kumwabudu.
10Kisha Yesu akawaambia: “Musiogope, muende kuwaambia wandugu zangu waende Galilaya, na kule wataniona.”
Waaskari wanaenda kupeleka habari11Wale wanawake walipokuwa wakienda, waaskari wamoja kati ya wale waliochunga kaburi wakaenda katika muji na kuwapasha wakubwa wa makuhani habari za mambo yote yaliyotokea.
12Wakubwa wa makuhani wakakutana pamoja na wasimamizi wa watu na kukata shauri. Wakawapa wale waaskari feza nyingi
13wakiwaambia: “Mutasema kwamba wanafunzi wake walikuja kuiba maiti yake usiku wakati mulipokuwa mukilala usingizi.
14Na kama liwali akisikia habari hii, sisi tutasemezana naye na kuhakikisha yale yaliyotokea kusudi musipate matata.”
15Basi wale waaskari walinzi wakapokea zile feza na kufanya sawa walivyoambiwa. Na habari hii ilienea katikati ya Wayuda mpaka leo.
Yesu anawatokea wanafunzi wake(Mk 16.14-18; Lk 24.36-49; Yn 20.19-23; Mdo 1.6-8)16Halafu wale wanafunzi kumi na mumoja wakaenda Galilaya kwa mulima ule Yesu aliowaagiza.
17Wakati walipomwona, wakamwabudu, lakini wamoja kati yao wakaona shaka.
18Kisha Yesu akakuja karibu nao, na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na katika dunia.
19Basi muwaendee watu wa mataifa yote kusudi wapate kuwa wanafunzi wangu, mukiwabatiza kwa jina la Baba, la Mwana na la Roho Mutakatifu.
20Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.