1Kisha Solomono akaanza kujenga nyumba ya Yawe katika Yerusalema juu ya mulima Moria ambapo Yawe alimutokea Daudi baba yake, pahali ambapo Daudi alikuwa amepachagua, kwenye kiwanja cha kupepetea ngano cha Ornani Muyebusi. Nguzo mbili za shaba(1 Fal 7.15-22)
15Mufalme Solomono alitengeneza nguzo mbili za shaba, kila moja yenye urefu wa metre mia moja kumi na tano na nusu, akaziweka mbele ya nyumba. Kisha akatengeneza taji mbili, kila moja yenye urefu wa metre mbili na sentimetre makumi mbili na tano, akaziweka juu ya nguzo zile.
16Alitengeneza minyororo kwa mufano wa mikufu, akaiweka juu ya vichwa vya nguzo hizo, kisha akatengeneza mifano ya matunda aina ya makomamanga mia moja, akayaweka juu ya minyororo hiyo.
17Akazisimamisha nguzo zile kwenye baraza ya hekalu, moja upande wa kusini, na ingine upande wa kaskazini; ile ya upande wa kusini akaiita Yakini, na ya upande wa kaskazini akaiita Boazi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.