Ezekieli 11 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Zambi ya Yerusalema

1Roho wa Mungu akaninyanyua na kunipeleka mpaka kwenye mulango wa upande wa mashariki wa nyumba ya Yawe. Huko nikawaona watu makumi mbili na watano. Kati yao kulikuwa Yazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, ambao ni wakubwa wa Waisraeli.

2Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu, hawa ndio watu wanaofanya mipango ya uovu na kutoa mashauri mabaya katika muji huu.

3Wanasema hivi: Wakati wa kujenga nyumba haujakaribia bado. Muji ni kama chungu kikubwa, na sisi ni kama nyama.

4Kwa hiyo, utoe unabii juu yao! Tabiri ewe mwanadamu!

5Kisha Roho wa Yawe akaniingia, naye akaniambia: Uwaambie watu kwamba:

Yawe anasema hivi: Ni hivi ndivyo munavyosema, enyi Waisraeli. Ninajua mambo munayofikiri juu yake ndani ya moyo wenu.

6Ninyi mumewaua watu wengi katika muji huu, na kujaza barabara zake na watu waliouawa.

7Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kweli, muji huu ni chungu, na wale waliouawa ndio nyama. Ninyi lazima mutaondolewa katika muji.

8Ninyi mumeogopa upanga? Basi, mimi nitaleta upanga juu yenu!

–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–

9Nitawatoa ndani ya muji na kuwatoa katika mikono ya watu wa mataifa mengine, nami nitawahukumu.

10Mutauawa kwa upanga, nami nitawahukumu katika inchi ya Waisraeli. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.

11Muji Yerusalema hautakuwa tena chungu chenu wala ninyi hamutakuwa nyama ndani yake. Mimi nitawahukumu katika inchi ya Waisraeli.

12Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe ambaye hamukufuata masharti yake na maagizo yake hamukuyatimiza, lakini mumetenda kufuatana na maagizo ya mataifa yanayowazunguka.

13Nilipokuwa ninatabiri, Pelatia mwana wa Benaya akakufa. Nami nikaanguka uso mpaka chini, nikalia kwa sauti kubwa, nikisema: Ee Bwana Yawe, utawamaliza kabisa Waisraeli waliobaki?

Ahadi ya Mungu kwa wanaokuwa katika uhamisho

14Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:

15Wewe mwanadamu, wandugu zako na wakaaji wa Yerusalema ambao vilevile ni wandugu zako wanasema juu yako na juu ya watu wote wa Israeli wanaokuwa katika uhamisho hivi: Ninyi munaokuwa katika uhamisho muko mbali sana na Yawe; maana Yawe ametupatia sisi inchi hii ikuwe mali yetu.

16Lakini, uwaambie hao wanaokuwa katika uhamisho kwamba Bwana wao Yawe anasema hivi: Ingawa nimewapeleka mbali kati ya mataifa na kuwasambaza katika inchi zingine, hata hivyo, mimi nipo pamoja nao huko wanakokuwa, kama vile hekalu kwao.

17Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitawakusanya toka kati ya watu, nitawakusanya kutoka katika inchi ambako mulisambazwa. Nitawarudisha katika inchi ya Israeli.

18Nanyi mutakaporudi katika inchi yenu nitaondoa vitu vyote vichafu na machukizo yote.

19Nitawapa moyo mupya na kuweka roho mupya ndani yenu. Nitauondoa ule moyo mugumu kama jiwe na kuwapa moyo musikilivu, Ang. Eze 36.26-28

20kusudi mupate kufuata masharti yangu na kuyatii maagizo yangu; nanyi mutakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu.

21Lakini hao ambao moyo wao umeambatana na vitu vichafu na machukizo yao, nitawaazibu kadiri ya mienendo yao.

–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.

Utukufu wa Mungu unatoka Yerusalema

22Halafu wale makerubi waliyakunjua mabawa yao na kuanza kuruka pamoja na yale magurudumu yaliyokuwa pembeni yao, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao. Ang. Eze 43.2-5

23Basi, utukufu wa Yawe ukapanda juu kutoka katikati ya muji, ukasimama juu ya mulima unaokuwa upande wa mashariki wa muji.

24Nikiwa katika maono hayo, Roho wa Mungu alininyanyua na kunipeleka mpaka katika inchi ya Babeli, kwa watu wanaokuwa kule katika uhamisho. Kisha maono hayo yakatoweka.

25Hapo nikawaelezea wale waliokuwa katika uhamisho mambo yote Yawe aliyonionyesha.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help