Hosea 12 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Watu wa Efuraimu wananizunguka kwa uongo,

na Waisraeli kwa udanganyifu.

Lakini watu wa Yuda wanaendelea kuwa mwaminifu kwa Mungu Mutakatifu.

2Watu wa Efuraimu wanachunga upepo,

muchana kutwa wanafukuza upepo wa mashariki.

Wanazidisha uongo na mateso,

wanafanya mapatano na Asuria

na kupeleka mafuta Misri.

3Yawe ana mashitaki juu ya Yuda;

atawaazibu wazao wa Yakobo kadiri ya makosa yao,

na kuwalipa kadiri ya matendo yao.

4Yakobo akiwa angali katika tumbo la mama yake,

alimushika kaka yake kisigino.

Na alipokuwa mutu muzima

alishindana na Mungu.

5Alipigana na malaika, akamushinda;

alilia machozi na kuomba ahurumiwe.

Kule Beteli, alikutana na Mungu,

na kusemezana naye,

6Yawe wa majeshi,

Yawe, ndilo jina lake.

7Lakini ninyi mumurudilie Mungu wenu.

Mushikamane na wema na haki,

mumutumainie Mungu wenu siku zote.

8Efuraimu ni sawa na muchuuzi

anayetumia vipimo vya udanganyifu,

anayependa kudanganya watu.

9Efuraimu amesema:

Mimi ni tajiri!

Mimi nimejitajirisha!

Sikufanya mabaya

kwa kupata hii faida.

10Yawe anasema: Mimi ni Yawe, Mungu wako,

tangia katika inchi ya Misri!

Mimi nitakukalisha tena katika mahema,

kama vile mulivyofanya

wakati nilipokutana nanyi.

11Mimi niliongea na manabii;

ni mimi niliyewapa maono mengi,

na kwa njia yao nilitangaza mupango wangu.

12Watu wa Gileadi walikuwa waovu sana;

hakuna tena kitu kinachokuwa chao.

Kule Gilgali walitambikia ngombe dume.

Hivyo, mazabahu zao zitakuwa malundo ya mawe

yaliyowekwa kwa mafungu katika shamba.

13Yakobo alikimbilia katika inchi ya Aramu.

Akiwa huko alifanya kazi kusudi apate mwanamuke,

akachunga kondoo kusudi apate mwanamuke.

14Kwa njia ya nabii, Yawe aliwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri.

Kwa njia ya nabii, Mungu aliwalinda.

15Waefuraimu wamemuchukiza Yawe sana.

Lakini Yawe atawalipiza makosa yao,

atawaazibu kwa mambo maovu waliyotenda.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help