Ezekieli 17 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mufano wa tai na muzabibu

1Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:

2Wewe mwanadamu! Tega kitendawili, uwaambie Waisraeli fumbo.

3Uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi:

Kulikuwa tai mumoja mukubwa sana

aliyekuwa na mabawa makubwa,

yenye manyoya marefu mengi

yenye rangi za kila aina.

Tai yule aliruka mpaka kwenye mulima Lebanoni,

akatua juu ya kilele cha muti wa mwerezi;

4akavunja tawi lake la juu zaidi,

akalipeleka katika inchi ya wachuuzi,

akaliweka katika muji wao mumoja.

5Kisha akatwaa kichipukizi cha mumea katika inchi ya Waisraeli,

akaupanda katika udongo wenye mboleo

ambako kulikuwa maji mengi.

6Mumea ukakomaa na kuwa muzabibu

wa aina ya muti unaotambaa;

matawi yake yakaelekea yule tai,

na mizizi yake ikaingia chini ndani ya udongo.

Muzabibu ukatoa matawi na majani mengi.

7Lakini kulikuwa tai mwingine mukubwa;

alikuwa na mabawa makubwa ya manyoya mengi.

Basi, ule muzabibu ulikunja mizizi yake,

ukamwelekezea matawi yake,

kusudi aumwangilie maji.

8Muzabibu ulikuwa umepandikizwa

penye udongo muzuri na karibu na maji mengi,

kusudi upate kutoa matawi na kuzaa matunda

uweze kuwa muzabibu muzuri sana!

9Sasa Bwana wenu Yawe anakuuliza:

Muzabibu huo utaweza kustawi?

Hawataongoa mizizi yake

na kuozesha matunda yake

na matawi yake machanga kuyanyausha?

Hakutahitajika mutu mwenye nguvu au kundi kubwa

kuuongoa kutoka ndani ya udongo.

10Umepandikizwa, lakini, utastawi?

Upepo mukali wa mashariki unapovuma juu yake utanyauka;

utakaukia palepale kwenye udongo ulikoota.

Maelezo yake

11Kisha neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:

12Sasa uwaulize wale watu waasi kama wanaelewa maana ya mufano huo. Uwaambie kwamba, mufalme wa Babeli alikuja Yerusalema, akamwondoa mufalme na wakubwa wake, akawapeleka Babeli. Ang. 2 Fal 24.15-20; 2 Sik 36.10-13

13Kisha akachagua mutu mumoja wa jamaa ya kifalme, akafanya naye mapatano, akamwapisha kiapo cha uaminifu. Aliwaondoa wakubwa wengine katika inchi akawapeleka mbali

14kusudi utawala huo ukuwe zaifu na ushike agano la mufalme wa Babeli.

15Lakini yule mufalme mupya alimwasi mufalme wa Babeli kwa kuwatuma wajumbe Misri kuomba farasi na waaskari wengi. Mufalme huyo atashinda? Anayefanya hivyo na kuvunja agano lake ataweza kuepuka azabu?

16Kama vile ninavyoishi, mufalme huyu atakufia katika inchi ya Babeli, inchi ya mufalme yule aliyemuweka kuwa mufalme, na ambaye amezarau kile kiapo na kuvunja lile agano alilofanya naye.

17Hakika, Mufalme wa Misri pamoja na jeshi lake kubwa hataweza kumusaidia katika vita wakati Wababeli watakapomuzungushia kikingio na kuta kusudi wapate kuwaua watu wengi.

18Kwa sababu alikizarau kile kiapo na kuvunja lile agano ambalo aliahidi kwa mukono wake mwenyewe na kufanya mambo yale yote, hakika hataokoka.

19Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kama vile ninavyoishi, nitamwazibu vikali kwa sababu amekizarau kiapo alichoapa kwa jina langu na kuvunja agano langu.

20Nitatandaza wavu wangu juu yake, naye atanaswa katika mutego wangu; nitamupeleka mpaka Babeli na kumuhukumu kwa sababu ya udanganyifu alioufanya juu yangu.

21Waaskari wake hodari watauawa kwa upanga na wale watakaoponyoka watatawanyika pande zote. Kwa hiyo mutatambua kwamba ni mimi, kweli ni mimi Yawe ninayesema hivyo.

Ahadi ya Mungu ya tumaini

22Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi mwenyewe nitatwaa kichipukizi cha incha ya juu ya muti wa mwerezi. Nitavunja tawi changa kutoka matawi yake ya juu na kulipanda juu ya mulima murefu sana.

23Kweli, nitalipanda juu ya mulima murefu wa inchi ya Waisraeli kusudi lichanue na kuzaa matunda. Litakuwa mwerezi muzuri, na ndege wa aina zote watakaa chini yake vilevile watajenga chicha zao katika matawi yake.

24Halafu miti yote katika inchi itajua kwamba mimi Yawe ninaishusha miti mirefu na kuinua miti mifupi. Mimi ninakausha miti mibichi na kustawisha miti yenye kukauka. Ni mimi Yawe ninayesema hayo na nitayafanya.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help