1Zaburi ya Wakora.
2Yawe, ni mukubwa; anastahili kusifiwa sana
katika muji wake, ndio mulima wake mutakatifu.
3Sayuni, mulima wa Mungu, unapendeza kwa urefu;
muji wa Mufalme mukubwa ni furaha ya ulimwengu.
4Mungu analinda pango zake za kukimbilia;
yeye anajulikana kuwa upango wake.
5Wafalme walikusanyika,
wakaenda pamoja kushambulia.
6Lakini walipouona Sayuni, wakashangaa;
wakashikwa na hofu na kukimbia.
7Hofu kubwa iliwashika,
wakasikia uchungu kama mama anayezaa,
8kama vile wenye kurushwa na upepo mukali wa mashariki,
ambao unavunjavunja mashua kubwa sana za Tarsisi.
9Yote tuliyosikia tumejionea wenyewe
katika muji wa Yawe wa majeshi,
katika muji wa Mungu wetu:
Mungu atauimarisha milele.
10Ee Mungu, tunakumbuka wema wako
tunapokuwa katika hekalu lako.
11Jina lako linasifiwa kila pahali,
sifa zako zinaenea fasi zote katika dunia.
Kwa mukono wako umetenda kwa haki.
12Watu wa Sayuni wafurahi!
Watu wa Yuda washangilie,
kwa sababu ya hukumu yako ya haki!
13Mutembee huko Sayuni, muuzunguke,
muihesabu minara yake.
14Muangalie kuta zake
na kuchunguza pango zake za kukimbilia,
mupate kuelezea vizazi vitakavyokuja kwamba:
15“Huyu ni Mungu, Mungu wetu milele!
Atakuwa mwongozi wetu milele!”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.