1Mufalme Nebukadneza wa Babeli alimusimika Zedekia mwana wa Yosia kuwa mufalme wa Yuda pahali pa Konia mwana wa Yoyakimu.
2Lakini Zedekia na wakubwa wake pamoja na wanainchi wa Yuda hawakusikiliza maonyo Yawe aliyotoa kwa njia ya nabii Yeremia.
3Mufalme Zedekia aliwatuma Yehukali mwana wa Selemia, pamoja na kuhani Zefania mwana wa Maseya, kwa nabii Yeremia kusema awaombee kwa Yawe, Mungu wao.
4Wakati huo, Yeremia alikuwa angali na uhuru wa kutembea kati ya watu, maana alikuwa hajatiwa katika kifungo.
5Tena waaskari wa mufalme wa Misri walikuwa wameondoka Misri, na waaskari wa Wakaldea walikuwa wameuzunguka Yerusalema waliposikia habari hizo waliondoka.
6Halafu neno la Yawe lilimufikia Yeremia kusema hivi:
7Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Utamwambia mufalme wa Yuda hivi ambaye amekutuma uniombe kwa ajili yake: Waaskari wa Mufalme wa Misri waliokuja kukusaidia, wako karibu kurudia kwao Misri.
8Na Wakaldea watarudi kuushambulia muji huu. Watauteka muji na kuuteketeza kwa moto.
9Yawe anasema hivi: Musijidanganye wenyewe na kusema kwamba waaskari wa Wakaldea wataondoka. Kweli hawataondoka.
10Hata kama mukiwashinda waaskari wote wa Wakaldea wanaopigana nanyi na kunabaki tu katika mahema yao wale walioumizwa, hao watasimama na kuuteketeza muji huu kwa moto.
Yeremia anatiwa katika kifungo11Kundi la waaskari wa Wakaldea lilipoondoka Yerusalema kwa kulikimbia kundi la waaskari wa mufalme wa Misri lililokuwa linakaribia,
12Yeremia aliondoka Yerusalema kwenda katika inchi ya Benjamina kwa kupokea sehemu ya urizi wake.
13Alipokuwa katika mulango wa Benjamina, mulinzi mumoja anayeitwa Iria mwana wa Selemia, mujukuu wa Hanania, alimukamata Yeremia na kumwambia: Wewe unatoroka kusudi uende kujiunga na Wakaldea!
14Yeremia akamwambia: Huo ni uongo! Mimi sitoroki na kwenda kujiunga na Wakaldea. Lakini Iria hakusadiki maneno ya Yeremia. Basi akamutia katika kifungo na kumupeleka kwa wakubwa.
15Wakubwa hao walimukasirikia sana Yeremia wakamupiga, kisha wakamufunga katika kifungo katika nyumba ya katibu Yonatani iliyokuwa imegeuzwa kuwa gereza.
16Yeremia alipokuwa amefungwa katika gereza kwa muda wa siku nyingi,
17mufalme Zedekia alimwita na kumukaribisha kwake. Mufalme akamwuliza kwa siri wakiwa katika nyumba yake: Kuna neno lolote kutoka kwa Yawe?
Yeremia akamujibu: Ndiyo, kuko. Kisha akaendelea kusema: Wewe utatiwa katika mikono ya mufalme wa Babeli.
18Halafu Yeremia akamwuliza mufalme Zedekia: Nimekukosea nini, au nimewakosea nini watumishi wako au watu hawa, hata unitie katika kifungo?
19Wako wapi manabii waliokutabiria wakisema: Mufalme wa Babeli hatakushambulia wewe wala inchi hii?
20Sasa ninakuomba unisikilize, ee bwana wangu mufalme. Ninakusihi sana ulikubali ombi langu. Tafazali usinirudishe tena katika kifungo katika nyumba ya katibu Yonatani, nisipate kukufia humo.
21Basi, mufalme Zedekia akatoa amri Yeremia awekwe katika chumba cha walinzi na kupewa mukate kila siku kutoka kwa wapikaji wa mukate mpaka mikate ilipotoweka kabisa huko katika muji. Basi, Yeremia alibaki katika chumba cha walinzi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.