Yobu 22 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Sehemu ya tatu ya Mazungumuzo(22.1–27.23)Masemi ya Elifasi

1Kisha Elifasi wa inchi ya Temani akajibu Yobu:

2Mwanadamu anafaa kwa kitu chochote mbele ya Mungu?

Kwa kweli mwenye hekima anajifaidia mwenyewe tu.

3Unazani kwamba unamufurahisha Mungu Mwenye Uwezo kama wewe ni mwenye haki?

Au anapata faida gani kama uko mukamilifu?

4Unazani anakuazibu na kukuhukumu

kwa sababu wewe unamuheshimu?

5Hapana! Uovu wako ni mukubwa sana!

Ubaya wako hauna mwisho!

6Wewe umemunyanganya ndugu yako nguo ya rehani;

umemutwaa nguo hiyo moja anayokuwa nayo.

7Umewanyima maji wale waliokuwa wamechoka;

umewanyima chakula wale wanaokuwa na njaa.

8Umemuruhusu mwenye cheo kunyanganya inchi yote;

umemwacha anayependelewa aishi mule.

9Umewaacha wajane waende mikono mitupu;

umewaponda wayatima mikono yao.

10Kwa hiyo mitego imekuzunguka pande zote,

hofu ya rafla imekupata.

11Giza limekuangukia usione kitu;

mafuriko ya maji yamekufunika.

12Tunajua kwamba Mungu yuko kule juu mbinguni;

Angalia jinsi nyota za juu kabisa zinavyokuwa mbali!

13Lakini wewe unasema: “Mungu anajua nini?

Anaweza kupenya mawingu na kutoa hukumu?

14Mawingu mazito yamemuzunguka asipate kuona;

anatembea inje ya anga la dunia!”

15Umeamua kufuata njia za zamani

ambazo watu waovu wamezifuata?

16Hao walifagiliwa mbele ya wakati wao,

misingi yao imepelekwa mbali na maji.

17Hao ndio waliomwambia Mungu: “Achana nasi!”

Na “Wewe Mungu Mwenye Uwezo unaweza nini juu yetu?”

18Lakini Mungu ndiye aliyejaza nyumba zao fanaka,

lakini walimuweka mbali na mipango yao!

19Wenye haki wanaona na kufurahi,

wasiokuwa na kosa wanawachekelea.

20Wanasema: kweli wale waadui zetu wameangamizwa,

na walichoacha kimeteketezwa kwa moto.

21Sasa, Yobu, ukubaliane na Mungu ukuwe na amani,

na kwa hiyo mazuri yatakufikia.

22Pokea mafundisho kutoka kwake;

na uyaweke maneno yake ndani ya moyo wako.

23Ukimurudilia Mungu na kunyenyekea,

ukiondoa uovu mbali na makao yako,

24ukitupilia mbali mali yako,

ukitupa zahabu ya Ofiri kwenye ukingo wa kijito,

25Mungu Mwenye Uwezo akiwa ndiyo zahabu yako

na feza yako ya bei kali,

26basi, ndipo utakapomufurahia Mungu Mwenye Uwezo

na kuinua uso wako kwake.

27Utamwomba naye atakusikiliza,

nawe utavitimiza viapo vyako.

28Neno lolote utakalokusudia litafanikiwa,

na mwangaza utaangazia njia zako.

29Maana, Mungu anawashusha wenye majivuno,

lakini anawaokoa wanyenyekevu.

30Yeye anamwokoa mutu asiyekuwa na kosa.

Nawe utaokolewa kwa sababu haukutenda mabaya.

Jibu la Yobu
Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help