1Katika mwezi wa kenda wa mwaka wa kenda wa utawala wa Zedekia mufalme wa Yuda, Nebukadneza mufalme wa Babeli alifika na waaskari wake wote kuushambulia Yerusalema, akauzunguka kwa vita.
2Na katika siku ya kenda ya mwezi wa ine, mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Zedekia, sehemu ya ukuta wa muji ilibomolewa.
3(Basi wakubwa hawa wote wa mufalme wa Babeli waliingia na kukaa kwenye mulango wa katikati: Nergali-Sarezeri, Samgari-Nebo, Sarsekimu jemadari mukubwa wa na Nergali-Sarezeri mukubwa wenye maarifa, pamoja na wakubwa wengine wote wa mufalme wa Babeli.)
4Naye Zedekia, mufalme wa Yuda na waaskari wake wote walipowaona, walitoroka. Walitoka inje ya muji usiku, wakipitia katika bustani ya mufalme, kwenye mulango katikati ya kuta mbili, wakatelemukia kwenye bonde la muto Yordani.
5Lakini kundi la waaskari la Wakaldea liliwafuatilia na kumukamata Zedekia karibu na Yeriko. Kisha kumukamata walimufikisha kwa Nebukadneza, mufalme wa Babeli huko Ribla, katika inchi ya Hamati, naye akamuhukumu.
6Kulekule Ribla, mufalme wa Babeli aliwaua wana wa Zedekia mbele ya baba yao. Waliwaua vilevile wakubwa wote wa Yuda.
7Kisha aliongoa macho ya Zedekia na kumufunga kwa minyororo, kusudi amupeleke Babeli.
8Wakaldea waliichoma kwa moto nyumba ya kifalme na nyumba za watu; vilevile walizibomoa kuta za Yerusalema.
9Kisha, Nebuzaradani, mukubwa wa walinzi wa mufalme, aliwapeleka katika uhamisho kule Babeli watu waliokuwa wamebaki katika muji na wale waliokuwa wamejitoa kwake pamoja na wafundi wote waliokuwa wamebaki.
10Nebuzaradani, mukubwa wa walinzi wa mufalme, aliwaacha katika inchi ya Yuda watu wamoja wamasikini ambao hawakukuwa na kitu chochote, akawagawanyia mashamba ya mizabibu na kuwapa maeneo ya kulima wakati huohuo.
Yeremia anafunguliwa11Nebukadneza mufalme wa Babeli alikuwa amemupa Nebuzaradani mukubwa wa walinzi, amri hii juu ya Yeremia:
12Umutwae Yeremia, umutunze vema wala usimuzuru; umutendee kama anavyokuambia.
13Basi, Nebuzaradani mukubwa wa walinzi, Nebusazibani, Nergali-Sarezeri pamoja na wakubwa wote wa mufalme wa Babeli, wakatuma watu wamwondoe Yeremia katika chumba cha walinzi.
14Wakamutoa Yeremia kwa Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu, amupeleke katika nyumba yake. Basi, Yeremia akaishi pamoja na wanainchi wengine.
Tumaini la Ebedimeleki15Wakati Yeremia alipokuwa amefungwa katika chumba cha walinzi, neno la Yawe lilimufikia kusema hivi:
16Kwenda kwa Ebedimeleki Mwetiopia umwambie hivi:
Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Angalia mimi nitatimiza mambo yale niliyosema juu ya muji huo na sio mambo mema. Mambo hayo yatakamilika siku hiyo ukiona wewe mwenyewe.
17Lakini siku hiyo mimi nitakuokoa wewe, wala hautatiwa katika mikono ya watu unaowaogopa.
18Maana, kweli nitakuokoa na hautauawa kwa vita; utapata faida ya kuokoa maisha yako kwa sababu umeniamini mimi.
–Ni ujumbe wa Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.