1Kisha Waisraeli wote walikusanyika mbele ya Daudi kule Hebroni, wakamwambia: “Sisi ni mwili na damu yako.
2Zamani, Saulo alipokuwa mufalme wewe ndiwe uliyewaongoza Waisraeli katika vita, na Yawe, Mungu wako alikuambia: ‘Utakuwa muchungaji wa watu wangu Waisraeli, na utakuwa mukubwa wa watu wangu Waisraeli.’ ”
3Basi, wazee wote wa Waisraeli wakamwendea mufalme kule Hebroni; naye Daudi akafanya agano nao mbele ya Yawe, halafu wakamupakaa Daudi mafuta akuwe mufalme wa Waisraeli kulingana na neno la Yawe lililotolewa kwa njia ya Samweli.
4Nyuma ya hayo Daudi na Waisraeli wote walikwenda Yerusalema, muji uliojulikana kwa jina la Yebusi, na ambao wenyeji wake walikuwa Wayebusi. Yeye alipigana kwa mukuki wake akaua watu mia tatu kwa mara moja katika vita.
12Halafu aliyefuata kati ya wale mashujaa watatu alikuwa Eleazari mwana wa Dodo, wa ukoo wa Ahoa.
13Siku moja Eleazari alikuwa pamoja na Daudi kule Pasi-Damimu, wakati Wafilistini walipokusanyika kupigana vita. Kule kulikuwa shamba lenye shayiri tele, lakini Waisraeli wakawakimbia Wafilistini.
14Lakini wakasimama imara katikati ya shamba lile kwa kulikinga, wakaua Wafilistini; Yawe akawaokoa kwa kuwapa ushindi mukubwa.
15Kisha mashujaa watatu kati ya wakubwa makumi tatu wakamwendea Daudi kwenye mulima wa pango la Adulamu. Wakati ule jeshi la Wafilistini lilikuwa limepiga kambi katika bonde la Refaimu.
16Naye Daudi wakati ule alikuwa katika maficho, nalo jeshi la Wafilistini lilikuwa katika muji wa Betelehemu.
17Daudi akapatwa na hamu kubwa akasema: “Heri kama mutu angeweza kunipa maji ya kunywa kutoka katika kisima cha Betelehemu kinachokuwa karibu na mulango wa muji!”
18Wale mashujaa wake watatu wakatoka, wakapenya katikati ya kambi ya jeshi la Wafilistini, wakaenda na kuchota maji katika kisima cha Betelehemu, karibu na mulango wa muji, wakamuletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyakunywa, na kwa pahali pake akayamwanga chini kama sadaka kwa Yawe
19akisema: “Tendo kama hili lipite mbali nami; siwezi kulifanya mbele ya Mungu wangu. Basi ninaweza kunywa damu ya maisha ya watu hawa? Maana kwa kuyahatarisha maisha yao walileta maji haya.” Kwa hiyo Daudi hakukunywa maji yale. Hayo ndiyo mambo waliyotenda wale mashujaa watatu.
20Abisai, ndugu ya Yoabu, alikuwa mukubwa wa mashujaa makumi tatu. Yeye alipigana kwa mukuki wake na watu mia tatu, akawaua, akajipatia jina kati ya wale mashujaa watatu.
21Basi, akaheshimiwa zaidi kati ya mashujaa makumi tatu, hata akakuwa jemadari wao, lakini hakukuwa shujaa kama wale mashujaa watatu.
22Benaya mwana wa Yehoyada, kutoka muji wa Kabuseli, alikuwa askari shujaa ambaye alifanya mambo mengi ya ajabu. Aliua mashujaa wawili kutoka Moabu, na siku moja wakati wa baridi kali, akashuka na kuua simba ndani ya shimo.
23Vilevile, akamwua Mumisri mumoja, urefu wake ulikuwa metre mbili na nusu, naye alikuwa akibeba mukuki mukubwa sana katika mukono wake, kama muti wa mufumaji wa nguo. Lakini Benaya akamushambulia akiwa na fimbo tu, akamunyanganya mukuki ule, na kumwua Mumisri yule kwa mukuki wake mwenyewe.
24Benaya mwana wa Yehoyada alifanya mambo hayo, akajipatia sifa kati ya wale mashujaa watatu.
25Basi, akakuwa mwenye heshima kati ya wale mashujaa makumi tatu, ingawa hakukuwa shujaa kama wale mashujaa watatu. Na Daudi akamupa cheo cha mukubwa wa walinzi wake wa kipekee.
26-47Hawa ndio waaskari shujaa wa Daudi:
Asaheli ndugu ya Yoabu,
Elihanani mwana wa Dodo, wa Betelehemu,
Samoti wa Harodi,
Helesi wa Peloni,
Ira mwana wa Ikesi wa Tekoa,
Abiezeri wa Anatoti,
Sibekai wa Husa,
Ilai wa Ahohi,
Maharai wa Netofati,
Heledu mwana wa Bana wa Netofati,
Itai mwana wa Ribai, kutoka Gibea katika kabila la Benjamina,
Benaya wa Piratoni,
Hurai kutoka vijito vya Gasi,
Abieli wa Araba,
Azimaweti wa Baharumu,
Eliaba wa Salaboni, wana wa Yaseni wa Gizoni,
Yonatani mwana wa Sage wa Harari,
Ahiyamu mwana wa Sakari wa Harari,
Elifali mwana wa Uri,
Heferi wa Mekerati,
Ahiya wa Peloni,
Hesero wa Karmeli,
Naarai mwana wa Esibai,
Yoeli ndugu ya Natani,
Mibuhari mwana wa Hagiri,
Zeleki wa Amoni,
Naharai wa Beroti aliyekuwa mubebaji wa silaha wa Yoabu mwana wa Zeruya,
Ira na Garebu, waliokuwa wa Itiri,
Uria Muhiti,
Zabadi mwana wa Alai,
Adina mwana wa Siza wa kabila la Rubeni, mukubwa wa kabila la Rubeni, akiwa pamoja na watu makumi tatu,
Hanani mwana wa Maka,
Yosafati wa Miti,
Usia wa Astera,
Sama na Yeieli, wana wa Hotamu wa Aroeri,
Yediaeli na ndugu yake Yoha, wana wa Simuri wa Tisi,
Elieli wa Mahawi,
Yeribali na Yosawia wana wa Elenama,
Itima wa inchi ya Moabu,
Elieli, Obedi, na Yasieli wa Mesoba.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.