1Wakati Ezra alipokuwa anaomba na kuungama naye akilia na kujiangusha uso mpaka chini mbele ya nyumba ya Mungu, kundi kubwa la watu wa Israeli, wanaume, wanawake na watoto, wakakusanyika karibu naye wakilia kwa uchungu mwingi.
2Halafu Sekania mwana wa Yehieli, wa ukoo wa Elamu, akamwambia Ezra: “Tumekosa uaminifu kwa Mungu kwa kuoa wanawake wa kigeni wa inchi hii, lakini hata hivyo bado kuna tumaini kwa ajili ya Israeli.
3Kwa hiyo, tufanye agano na Mungu wetu, tuachane na wanawake hawa pamoja na watoto wao, kwa kufuatana na shauri lako na la wengine wanaotii amri za Mungu. Yote yatendeke kwa kufuatana na Sheria.
4Amuka utende, sisi tutakuunga mukono. Kwa hiyo ujipe moyo ufanye hivyo.”
5Ezra akasimama na kuanza kuwaapiza makuhani, viongozi, Walawi na Waisraeli wengine wote kwamba watafanya kama ilivyosemwa, nao wakakubali kufanya kiapo.
6Kisha, Ezra akaondoka mbele ya nyumba ya Mungu, akaenda kwa nyumba ya Yehohanani mwana wa Eliasibu. Kule, Ezra akalala usiku kucha bila kula wala kunywa maji, kwa huzuni aliyokuwa nayo juu ya ukosefu wa imani ya watu waliotoka katika uhamisho.
7Tangazo likatolewa kila pahali katika inchi ya Yuda na Yerusalema kwa wote waliotoka katika uhamisho kwamba wakusanyike Yerusalema.
8Ikiwa mutu yeyote atashindwa kufika katika muda wa siku tatu, kulingana na amri iliyotolewa na viongozi, mali yake yote itanyanganywa, naye mwenyewe atatengwa mbali na makutano na jamii ya watu waliorudi kutoka katika uhamisho.
9Katika siku hizo tatu, kwa siku ya makumi mbili ya mwezi wa tisa, watu wote walioishi katika majimbo ya Yuda na Benjamina wakafika Yerusalema na kukusanyika katika kiwanja cha nyumba ya Mungu. Watu wote walikuwa wakitetemeka kwa sababu ya shauri waliloitiwa na kwa ajili ya mvua nyingi iliyokuwa ikinyesha.
10Kuhani Ezra akasimama kwa kuzungumuza na watu, akawaambia: “Hamukukuwa waaminifu kwa kuoa wanawake wa kigeni, na hivyo mumeiongezea Israeli kosa.
11Sasa, mutubu zambi zenu mbele ya Yawe, Mungu wa babu zenu, na kufanya yale yanayomupendeza. Mujitenge na wakaaji wa inchi hii na kuwaacha wake zenu wa kigeni.”
12Watu wote wakasema kwa sauti na kujibu kwa pamoja: “Ni sawa! Tunapaswa kufanya kama vile unavyosema.”
13Lakini wakaongeza kusema: “Watu ni wengi na mvua inanyesha sana. Hatuwezi kuendelea kusimama hapa katika kiwanja, na hili si jambo ambalo litamalizika kwa siku moja au mbili! Tumefanya kosa kubwa sana juu ya shauri hili.
14Afazali wakubwa wetu wabaki Yerusalema kushugulikia jambo hili kwa ajili ya watu wote. Kisha, kila mumoja ambaye ameoa mwanamuke wa kigeni akuje kwa zamu pamoja na viongozi na waamuzi wa muji wake, mpaka pale kasirani kali ya Mungu wetu itakapoondolewa kwetu.”
15Hakuna aliyepinga mupango huu, isipokuwa tu Yonatani mwana wa Asaeli na Yazeya mwana wa Tikwa, nao wakaungwa mukono na Mesulamu na Mulawi Sabetayi.
16Watu wote waliorudi kutoka katika uhamisho wakakubali mupango huo, kwa hiyo kuhani Ezra akawachagua wanaume kati ya viongozi wa ukoo mbalimbali na kuyaandika majina yao. Kwa siku ya kwanza ya mwezi wa kumi, watu hao wakaanza kazi yao ya uchunguzi wa shauri hilo.
17Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, walikuwa wamekwisha kumaliza uchunguzi wao juu ya wanaume wote waliokuwa wameoa wanawake wa kigeni.
Wanaume waliooa wanawake wa kigeni18Hawa ndio makuhani waliooa wanawake wa kigeni:
Wazao wa Yesua, wana wa Yehosadaki na wandugu zake: Maseya, Eliezeri, Yaribu na Gedalia.
19Hao waliahidi kuwaacha wake zao, na wakatoa kondoo dume kuwa sadaka kwa ajili ya kosa yao.
20Wazao wa Imeri: Hanani na Zebadia.
21Wazao wa Harimu: Maseya, Elia, Semaya, Yehieli na Uzia.
22Wazao wa Pashuri: Eliyoenayi, Maseya, Isimaeli, Netaneli, Yozabadi na Elasa.
23Kati ya Walawi kulikuwa: Yozabadi, Simei, Kelaya (aliyejulikana pia kwa jina la Kelita), Petahia, Yuda na Eliezeri.
24Kati ya waimbaji kulikuwa: Eliasibu. Walinzi wa milango: Salumu, Telemu na Uri.
25Kati ya watu wengine wa Israeli kulikuwa:
Wazao wa Parosi: Ramia, Izia, Malkia, Miyamini, Eleazari, Malkia na Benaya.
26Wazao wa Elamu: Matania, Zakaria, Yehieli Abudi, Yeremoti na Elia.
27Wazao wa Zatu: Eliyoenayi, Eliasibu, Matania, Yeremoti, Zabadi na Aziza.
28Wazao wa Bebayi: Yehohanani, Hanania, Zabayi na Atilayi.
29Wazao wa Bani: Mesulamu, Maluki, Adaya, Yasubu, Seali na Yeremoti.
30Wazao wa Pahati-Moabu: Adina, Kelali, Benaya, Maseya, Matania, Besaleli, Binui na Manase.
31Wazao wa Harimu: Eliezeri, Isia, Malkia, Semaya, Simeoni,
32Benjamina, Maluki na Semaria.
33Wazao wa Hasumu: Matenayi, Matata, Zabadi, Elifeleti, Yeremayi, Manase na Simei.
34Wazao wa Bani: Madayi, Amuramu, Ueli,
35Benaya, Bedeya, Keluhi,
36Wania, Meremoti, Eliasibu,
37Matania, Matenayi na Yasu.
38Wazao wa Binui: Simei,
39Selemia, Natani, Adaya,
40Makinadebayi, Sasayi, Sarai,
41Azareli, Selemia, Semaria,
42Salumu, Amaria na Yosefu.
43Wazao wa Nebo: Yeieli, Matitia, Zabadi, Zebina, Yadai, Yoeli na Benaya.
44Hao wote walioa wanawake wa kigeni na wamoja kati yao walizaa na wanawake wale.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.