1“Ukimwona ngombe au kondoo wa ndugu yako amepotea, usimwache, lakini umurudishe kwa ndugu yako.
2Lakini kama nyumba ya huyu ndugu si karibu au kama haumujui mwenyeji, basi, utatwaa nyama huyo kwako, akae kwako mpaka mwenyeji atakapokuja, nawe utamurudishia naye.
3Utafanya vivyo hivyo kwa punda au vazi au kitu chochote ambacho ndugu yako amekipoteza. Usiache kumusaidia.
4“Ukiona punda au ngombe wa ndugu yako ameanguka katika njia, usiache kumusaidia ndugu yako; utamusaidia kumwinua.
5“Wanawake wasivae nguo za wanaume, na wanaume wasivae nguo za wanawake. Anayefanya hivyo ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu.
6“Ukikuta chicha ya ndege juu ya muti au katika njia, inayokuwa na vitoto au mayai na mama ndege amefunika hivyo vitoto au mayai, usitwae mama ndege na vitoto vyake.
7Utamwacha mama ndege aende zake, lakini unaweza kutwaa vitoto. Ukifanya hivyo utafanikiwa na kuishi maisha marefu.
8“Unapojenga nyumba, jenga ukuta pembeni ya paa, kusudi usihukumiwe kama mutu akianguka kutoka huko, na kufa.
9“Usipande mizabibu yako pamoja na mimea mingine, kama sivyo mazao yote yatakuwa haramu, siyo tu yale uliyopanda lakini vilevile matunda ya mizabibu.
10“Usilime shamba kwa kutumia ngombe na punda pamoja.
11“Usivae nguo zilizofumwa kwa sufu na kitani.
12“Funga vishada katika pembe ine za nguo yako.
Heshima juu ya mambo ya mume na muke13“Kama mwanaume anamwoa mwanamuke, halafu kisha akakata shauri la kumwacha,
14na kumushitaki kwamba ametenda mambo ya haya, na kumuharibishia sifa yake kwa kusema kwamba hakukuwa bikira wakati alipomwoa,
15basi, kama ikitokea hivyo, wazazi wa huyo binti watapeleka ushuhuda wa ubikira wa binti yao kwa wazee kwenye mulango wa muji na kuwaambia:
16‘Tulimwoesha binti yetu huyu kwa mutu huyu, lakini sasa hamutaki tena,
17na ajabu ni kwamba ameshitaki mambo ya haya na kusema kwamba hakumukuta na ushuhuda wowote kwamba alikuwa bikira. Hata hivyo ushuhuda wa ubikira wa binti yetu ni huu’. Halafu atakunjua nguo yenye huo ushuhuda mbele ya wazee wa muji.
18Hapo wazee wa muji watamupeleka yule mwanaume na kumwazibu.
19Vilevile watamulipisha mutu huyo malipo ya vikoroti mia moja vya feza na kupewa baba wa huyo mwanamuke kwa sababu mwanaume huyo amemuharibishia binti wa Israeli sifa. Na huyo mwanamuke ataendelea kuwa muke wake na hataweza kuachana naye maisha yake yote.
20Lakini kama mashitaki hayo ni ya kweli, na hakuna ushuhuda wa ubikira wake,
21watamupeleka kwenye mulango wa nyumba ya baba yake na wanaume wa muji huo watamupiga mawe akufe, kwa sababu amefanya upumbafu katika Israeli kwa kufanya ukahaba akiwa katika nyumba ya baba yake. Ndivyo mutakavyokomesha uovu huo kati yenu.
22“Mutu akikamatwa akilala na muke wa mutu mwingine, wote wawili, mwanaume na mwanamuke, wanapaswa kuuawa. Ndivyo mutakavyokomesha uovu huo kati yenu.
23“Mwanaume akimukuta binti aliyechumbiwa, akilala naye,
24mutawatoa wote wawili inje ya muji na kuwapiga mawe mpaka wakufe. Binti huyo anapaswa kuuawa kwa sababu hakupiga kelele kusudi asaidiwe ingawa alikuwa ndani ya muji; naye mwanaume anapaswa kuuawa kwa sababu amemuchafua muchumba wa mwenzake. Ndivyo mutakavyokomesha uovu huo kati yenu.
25“Lakini kama mwanaume amekutana na binti aliyechumbiwa akamushika kwa nguvu, basi ni huyo mwanaume tu atakayeuawa.
26Musimutendee huyo binti chochote; yeye hana kosa linalostahili azabu ya kifo. Tukio hili ni sawa na la mutu anayemushambulia mutu mwingine na kumwua, kwa sababu
27mwanaume huyo alimushika kwa nguvu huyo binti huko katika mbuga, na ingawa alipiga kelele kwa kuomba musaada hakukuwa mutu wa kumusaidia.
28“Mwanaume akikutana na binti ambaye hajachumbiwa, akimushika kwa nguvu, wakikamatwa,
29mwanaume huyo atamulipa baba wa binti huyo vikoroti makumi tano vya feza kwa sababu amemuchafua, na binti huyo atakuwa muke wake na hatamwacha maisha yake yote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.