Danieli 1 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Danieli na wenzake katika nyumba ya mufalme

1Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Yoyakimu wa Yuda, mufalme Nebukadneza wa Babeli alikwenda Yerusalema, akauzunguka muji.

3Mufalme Nebukadneza akamwamuru Aspenazi, mukubwa wa watumishi wake, amuchagulie kati ya vijana wa Waisraeli wa jamaa ya kifalme na ya watu wenye heshima.

4Mufalme alitaka vijana wasiokuwa na kilema, wazuri kwa umbo, wenye ujuzi wa kila hekima, wenye akili na maarifa na wanaofaa kwa kutumika katika nyumba ya kifalme. Alitaka vilevile vijana wale wafundishwe kusoma na kuandika luga ya Wakaldea.

5Mufalme aliagiza vijana wale wapewe chakula bora ambacho yeye mwenyewe alikula na divai ambayo alikunywa. Aliagiza vilevile vijana wale wafundishwe kwa miaka mitatu, kisha wapelekwe kwa mufalme.

6Kati ya vijana waliochaguliwa kulikuwa Danieli, Hanania, Misaeli na Azaria, wote wa kabila la Yuda.

7Yule mukubwa wa watumishi akawapa majina mengine; akamwita Danieli kwa jina la Beltesaza, Hanania kwa jina la Sadiraki, Misaeli kwa jina la Mesaki na Azaria kwa jina la Abedenego.

8Lakini Danieli aliamua kutojichafua kwa kula chakula bora cha mufalme na kunywa divai yake. Kwa hiyo, alimwomba yule mukubwa amuruhusu asikule vitu hivyo na kujichafua.

9Basi, Mungu akamujalia Danieli kupendelewa na kuhurumiwa na Aspenazi, yule mukubwa.

10Lakini, mukubwa yule akamwambia Danieli: Ninaogopa kwamba bwana wangu mufalme ambaye ametoa maagizo juu ya chakula na kinywaji unavyopaswa kutumia, ataona kwamba afya yako si nzuri kama ya wenzako wa umri wako. Hivyo maisha yangu yatakuwa katika hatari.

11Halafu Danieli akamwendea mutumishi aliyewekwa na mukubwa yule kwa kumulinda yeye na wenzake watatu Hanania, Misaeli na Azaria, akamwambia:

12Tafazali utujaribu, sisi watumishi wako kwa muda wa siku kumi kwa kutupatia mboga za majani na maji.

13Kisha, utulinganishe sisi na hao vijana wengine wanaokula chakula cha mufalme, halafu utoe uamuzi wako kulingana na jinsi utakavyoona.

14Mulinzi akakubaliana nao, akawajaribu kwa muda wa siku kumi.

15Kisha siku hizo kumi, aliwaangalia akaona kwamba wale vijana waliokula mboga za majani walionekana wenye afya na nguvu kuliko wale wengine wote waliokulishwa chakula cha kifalme.

16Basi, yule mulinzi akawaacha waendelee kula mboga za majani pahali pa chakula na divai walioamuriwa.

17Mungu aliwajalia vijana wale wane maarifa na ujuzi katika elimu na hekima. Zaidi ya hayo, alimujalia Danieli ufahamu wa kufasiria maono na ndoto.

18Muda ulipotimia ambapo wale vijana wangepelekwa kwa mufalme kama alivyokuwa ameagiza, yule mukubwa akawapeleka vijana wote mbele ya Nebukadneza.

19Mufalme alipozungumuza nao wote, hakuna walioonekana kuwa bora kama Danieli, Hanania, Misaeli na Azaria. Basi, wakakubaliwa kumutumikia mufalme.

20Jambo lolote la hekima au la maarifa ambalo mufalme aliwauliza alijionea mwenyewe kwamba vijana wale wane walikuwa bora mara kumi kuliko waaguzi na wachawi wote katika utawala wake.

21Danieli alidumu katika kazi ya nyumba ya mufalme mpaka mwaka wa kwanza wa utawala wa mufalme Kiro.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help