1Katika siku kumi, ya mwezi wa kumi, kwa mwaka wa kenda tangu kuhamishwa kwetu, neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
2Wewe mwanadamu! Andika tarehe ya siku ya leo, maana hii ni siku ambapo mufalme wa Babeli anaanza kuushambulia Yerusalema. chini ya chungu,
tokotesha vipande vya nyama na mifupa,
vyote uvitokoteshe vizuri.
6Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ole kwake muji wa mauaji! Muji huo ni kama chungu chenye kutu, ambacho kutu yake haiwezi kutoka! Vipande vya nyama ndani yake vinatoshwa kimoja kimoja bila kuchaguliwa.
7Mauaji yako humo katika muji; damu yenyewe haikumwangwa juu ya udongo kusudi ifunikwe na mavumbi, lakini ilimwangwa juu ya jiwe.
8Damu hiyo nimeiacha huko juu ya jiwe kusudi isifunikwe, nipate kuamusha kasirani yangu na kulipiza kisasi.
9Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ole kwake muji wa mauaji! Mimi nitalundika lundo kubwa la kuni.
10Kusanya vipande vya kuni na kuwasha moto. Tokotesha nyama vizuri sana. Tokotesha na kukausha muchuzi, na mifupa ipate kuungua!
11Weka chungu kitupu juu ya makaa kipate moto sana, shaba yake ipate moto, uchafu wake uyeyushwe na kutu iunguzwe.
12Lakini ni kujisumbua bure; kutu yake nene haitoki hata kwa moto.
13Ewe Yerusalema, matendo yako machafu yamekuchafua. Ingawa nilijaribu kukutakasa, mwenyewe ulibaki muchafu. Basi, hautatakasika tena mpaka nitakapotuliza hasira yangu juu yako.
14Ni mimi Yawe ninayesema hivyo. Jambo hilo litakamilika; mimi nitalitenda. Sitajuta jambo hilo wala kukuonea huruma. Nitakuazibu kulingana na mwenendo na matendo yako. –Ni Bwana wetu Yawe anayesema hivyo.
Kifo cha muke wa nabii15Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
16Wewe mwanadamu! Kwa rafla nitakuondolea mupenzi wako. Lakini usiomboleze, wala kulia, wala kutoa machozi.
17Utaugua, lakini sio kwa sauti. Hautamufanyia kilio huyo aliyekufa. Vaa viatu vyako na kuvaa kitambaa; usiufunike uso wako wala kula chakula cha kilio.
18Basi, asubui nilisema na watu, na magaribi muke wangu akakufa. Na kesho yake asubui, nilifanya kama nilivyoamuriwa.
19Watu wakaniuliza hivi: Jambo hili unalofanya lina maana gani?
20Nikawajibu: Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
21Uwaambie Waisraeli kwamba:
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitalichafua hekalu langu, hiyo nyumba ambayo munajivunia na kuitegemea na ambao munafurahi sana kuiona.
22Ninyi mutafanya kama vile Ezekieli alivyofanya. Hamutazifunika nyuso zenu wala kula chakula cha kilio.
23Mutavaa vitambaa kwa kichwa na viatu; hamutaomboleza, wala kulia. Kutokana na maovu yenu, mutaregea na kuugua, kila mutu na mwenzake.
24Naye Ezekieli atakuwa kitambulisho kwenu: mutafanya kila kitu kama vile alivyotenda. Wakati mambo hayo yatakapotukia, mutatambua kwamba mimi ni Bwana wenu Yawe.
25Yawe akaniambia hivi: Wewe mwanadamu! Siku ile nitakapoondoa kwao hicho ambacho ni tegemeo lao, na sababu ya shangwe yao, pahali ambapo wanapenda sana kupaona, nitawaondoa wana wao na wabinti zao.
26Siku hiyo, mutu atakayeponyoka atakuja kukupasha habari hizo.
27Siku hiyohiyo, utaacha kuwa bubu, nawe utaweza kuongea naye. Kwa hiyo wewe utakuwa kitambulisho kwao, nao watatambua kwamba mimi ni Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.