1Basi nitaendelea kujivuna ijapokuwa si vizuri. Lakini nitasema sasa juu ya maono na ufunuo nilivyopata toka kwa Bwana.
2Ninamujua mutu mumoja aliyeungana na Kristo, na sasa kumekwisha kupita miaka kumi na mine, mutu huyu akanyanyuliwa mpaka katika mbingu ya tatu. (Ikiwa alinyanyuliwa katika hali ya kimwili au ya kiroho mimi sijui, Mungu peke yake anajua.)
3Nami ninajua kwamba mutu yule alinyanyuliwa mpaka katika Paradizo. (Ninasema tena ikiwa mutu yule alinyanyuliwa katika hali ya kimwili au ya kiroho mimi sijui, Mungu peke yake anajua.)
4Katika Paradizo, mutu yule akasikia mambo ya ajabu na yasiyoruhusiwa kwa mwanadamu kuyaeleza.
5Basi, nitajivuna kwa ajili ya mutu sawa na yule, lakini sitajivuna kwa ajili yangu mimi mwenyewe, isipokuwa tu kwa ajili ya uzaifu wangu.
6Kama ningetaka kujivuna, singekuwa mupumbafu, maana ningesema tu ukweli. Lakini ninaepuka kujivuna, kusudi watu wasinihesabu kuwa mukubwa kuliko vile wanavyoona nikifanya au kunisikia nikisema.
7Lakini, kusudi nisijivune kupita kipimo kwa ajili ya kupokea ufunuo wa ajabu, nilitiwa katika mwili wangu kitu kinachoniumiza kama mwiba. Kitu kile ni kama mujumbe wa Shetani kwa kunipiga na kunizuiza nisijivune kupita kipimo.
8Nami nilimusihi Bwana mara tatu kusudi aniondolee kitu kile.
9Lakini akanijibu: “Neema yangu inakutoshelea, kwa maana uwezo wangu unatimizwa katika uzaifu.” Basi tafazali nijivunie sana uzaifu wangu kusudi nijazwe na uwezo wa Kristo.
10Kwa sababu hii ninafurahia uzaifu, matusi, ukosefu, taabu na mateso kwa ajili ya Kristo. Kwa maana wakati ninapokuwa muzaifu, basi ndio wakati ule ninapokuwa na nguvu.
Huzuni ya Paulo kwa Wakorinto11Ninasema kama mupumbafu, lakini ni ninyi ndio mumenilazimisha kufanya vile. Kufuatana na ile, ningepaswa kusifiwa nanyi. Kwa maana hata kama mimi si kitu, wale mitume wenu wanaohesabiwa kuwa wakubwa hawanipiti kitu kabisa.
12Matendo yanayohakikisha kwamba mimi ni mutume yamefanyika kati yenu kwa uvumilivu wote, kwa njia ya miujiza, maajabu, na vitambulisho.
13Mumepungukiwa na nini kuliko makanisa mengine, isipokuwa tu kwamba mimi sikuwalemea kwa kupata musaada toka kwenu? Munisamehe kwa kosa hili.
14Sasa mimi niko tayari kufika kwenu kwa mara ya tatu, nami sitawalemea. Maana sihitaji mali yenu, lakini ninawahitaji ninyi. Kwa sababu si kazi ya watoto kuwawekea wazazi wao akiba, lakini ni kazi ya wazazi kuwawekea watoto wao akiba.
15Kwa ngambo yangu, nitafurahi kutumia vyote ninavyokuwa navyo na kujitoa mimi mwenyewe, kwa ajili yenu. Ikiwa ninawapenda zaidi namna hii, hamupaswi kupungukiwa na upendo kwangu.
16Basi mutakubali kwamba mimi sikuwalemea. Lakini watu wengine wanafikiri kwamba mimi ni mwerevu na nimewanasa kwa kuwadanganya.
17Basi niliwaibia ninyi kwa njia ya mutu mumoja kati ya wale niliowatuma kwenu?
18Nilimusihi Tito aende kwenu na nimemutuma pamoja na ndugu mwingine. Munaweza kusema kwamba Tito amewaibia ninyi? Basi mimi pamoja naye tuliishi katika nia moja na kuwa na mwenendo mumoja.
19Ninyi munazani kwamba kwa wakati huu wote sisi tunajitetea mbele yenu? Tunasema mambo yale mbele ya Mungu kufuatana na vile tunavyoungana na Kristo. Wandugu wapendwa, mambo yale yote ni kwa kuwajenga ninyi katika imani.
20Kwa maana ninaogopa kwamba wakati ninapokuja kwenu, sitawakuta sawa vile ninavyotaka, nanyi hamutanikuta sawa vile munavyotaka. Ninaogopa kuwakuta katika fitina, wivu, kasirani, ugomvi, masingiziano, matetano, majivuno na fujo.
21Ninaogopa kwamba kwa safari yangu ingine, Mungu wangu atanifanya tena kuwa mwenye haya mbele yenu. Nami nitalia kwa ajili ya watu wengi waliofanya zambi zamani nao hawakugeuka toka katika uasherati, uzinzi na tamaa mbaya walizofanya.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.