Kutoka 25 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Matoleo kwa ajili ya hema takatifu(Kut 35.4-9)

1Yawe akamwambia Musa:

2Uwaambie Waisraeli wanipe michango ya matoleo. Utapokea matoleo kutoka kwa mutu yeyote atakayetoa kwa moyo safi.

3Utapokea matoleo haya: zahabu, feza, shaba,

4sufu ya samawi, ya zambarau na nyekundu, kitani safi iliyosokotwa na manyoya ya mbuzi;

5ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, ngozi za mbuzi, mbao za mujohoro,

6mafuta kwa ajili ya taa, viungo kwa ajili ya mafuta ya kupakaa na kwa ajili ya ubani wenye harufu nzuri,

7mawe ya sardoniki, na mawe mengine kwa ajili ya mapambo ya kizibao cha kuhani na kifuko cha kifua.

8Vilevile Waisraeli watanitengenezea hema takatifu, kusudi niweze kukaa kati yao.

9Utatengeneza hema hiyo na vifaa vyake kulingana na mufano nitakaokuonyesha.

Sanduku la Agano(Kut 37.1-9)

10Waisraeli watengeneze sanduku la mbao za mujohoro, lenye urefu wa sentimetre mia moja na kumi, upana sentimetre makumi sita na sita, na urefu kwenda juu sentimetre makumi sita na sita.

11Utapaka sanduku lile zahabu safi ndani na inje na kulifanyia ukingo wa zahabu pande zote.

12Kisha utalitengenezea pete ine na kuzitia kwenye miguu yake, kila muguu pete moja.

13Utachonga miti ya mujohoro na kuipakaa zahabu.

14Miti ile utaipitisha katika pete zinazokuwa kwa pande mbili za sanduku, kwa ajili ya kulibeba.

15Miti ile itabaki siku zote katika pete. Isitolewe wakati wowote.

16Ndani ya sanduku hilo utaweka vibao vya mawe vya agano.

17Kisha utatengeneza kiti cha rehema cha zahabu safi, urefu wake sentimetre mia moja na kumi, na upana wake sentimetre makumi sita na sita.

18Utatengeneza vilevile mufano wa makerubi wawili kwa kufua zahabu, uwaweke kwenye miisho miwili ya kiti kile;

19kerubi mumoja kwa mwisho mumoja na kerubi mwingine kwa mwisho mwingine. Uwaweke makerubi wale kwenye miisho ya kiti kile, lakini wakuwe kitu kimoja na kile kiti.

20Makerubi wale wataelekeana, mabawa yao yakikunjuka kukifunika kiti cha rehema. Nyuso zao zitaelekea kiti kile.

21Ndani ya sanduku utaweka vibao vya amri na kuweka kiti cha rehema juu yake.

22Mimi nitakutana nawe pale. Kutoka juu ya kiti kile cha rehema katikati ya makerubi wale wanaokuwa juu ya Sanduku la Agano, nitazungumuza nawe na kukupa amri zote kwa ajili ya Waisraeli.

Meza ya mikate iliyotolewa kwa Yawe(Kut 37.10-16)

23Utatengeneza meza ya mbao za mujohoro yenye urefu wa sentimetre makumi nane na nane, upana sentimetre makumi ine na ine na urefu kwenda juu sentimetre makumi sita na sita.

24Ile meza utaipakaa zahabu safi na kuizungushia ukingo wa zahabu.

25Kisha utaizungushia ubao wenye upana wa sentimetre makumi sita na sita na utaufanyia vilevile ukingo wa zahabu.

26Utaitengenezea pete ine za zahabu na kuzitia kwenye pembe zake kwenye miguu yake.

27Pete hizo zitakuwa karibu na ule ubao wa kuzunguka meza na zitakuwa za kuingizia ile miti ya kubebea ile meza.

28Utachonga miti ya mujohoro na kuipakaa zahabu. Miti itakuwa ya kubebea ile meza.

29Utatengeneza kwa ajili yake: sahani na vikombe vya kuwekea ubani na vilevile makopo na bakuli za kumiminia sadaka za kinywaji. Ufanye vyombo hivyo vyote kwa zahabu safi.

30Meza hiyo utaiweka mbele ya Sanduku la Agano na juu ya meza ile utaweka ile mikate muliyonitolea. Mikate ile itakuwa siku zote mbele yangu. Kinata cha taa(Kut 37.17-24)

31Utatengeneza kinara cha taa kwa zahabu safi. Tako lake na muti wa kile kinara vitakuwa kitu kimoja, vilevile na vikombe vyake. Mafundo yake na maua yake, vyote vitafuliwa kwa kipande kimoja tu cha zahabu.

32Matawi sita yatatokeza kila upande wa muti wake, matawi matatu upande mumoja na matawi matatu upande mwingine.

33Katika kila tawi kutakuwa vikombe vitatu mufano wa maua ya lozi, kila kimoja na kifundo chake na ua lake.

34Na katika muti kutakuwa vikombe vine mufano wa maua ya lozi, pamoja na vifundo vyake na maua yake.

35Na kutakuwa kifundo kila pahali matawi mawilimawili yanapotokea kufuatana na yale matawi sita yanayotokea kwa kile kinara.

36Vifundo hivyo na matawi yake yatakuwa kitu kimoja na kinara kile na chote kitafuliwa kwa zahabu safi.

37Utatengeneza vilevile taa saba kwa ajili ya kinara kile na kuziweka juu yake kusudi ziangaze kwa mbele.

38Tengeneza vilevile koleo zake na visahani vyake kwa zahabu safi.

39Utatumia kilo makumi tatu na tano za zahabu safi kwa kutengeneza kinara kile na vifaa vyake.

40Hakikisha kwamba umevitengeneza kwa mufano ulioonyeshwa kule juu ya mulima.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help