Ufunuo 18 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Uharibifu wa muji Babeli

1Kisha mambo hayo, nikaona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni. Yeye alikuwa na uwezo mukubwa; na dunia yote ilingaa kwa utukufu wake.

2Halafu akalalamika kwa sauti kubwa, akisema: “Umebomoka, umebomoka kabisa ule muji mukubwa Babeli! Sasa umekuwa makao ya mashetani ya kila namna, ya pepo wachafu, na makimbilio ya ndege wote wachafu na wenye kuchukiza.

3Ni kwa sababu mataifa yote yalileweshwa na divai kali ya uasherati wa muji ule. Wafalme wa dunia wamezini nao, na wachuuzi wa dunia wamejitajirisha kutokana na uwingi wa mali zake.”

4Kisha nikasikia sauti ingine kutoka mbinguni ikisema: “Mutoke katika muji ule ninyi watu wangu, kusudi musishiriki zambi zake na kupatwa vilevile na mapigo yatakayoupata.

5Kwa maana zambi zake zinazidi sana hata zimefika mbinguni na Mungu hakusahau mabaya yake.

6Mutendee muji ule sawa vile ulivyowatendea. Mulipize matendo yake mara mbili zaidi. Na katika kile kikombe alimochanganya divai yake, mumuchangie divai inayokuwa kali mara mbili zaidi kuliko ile aliyowapa.

7Na kwa kadiri ulivyojitukuza na kuishi katika raha, kwa kadiri ile ile muuletee mateso na huzuni. Muji ule unajisemesha: ‘Mimi ninaikaa juu ya kiti cha kifalme kama vile malkia; mimi si mujane, wala sitapata huzuni hata kidogo!’

8Kwa sababu hiyo, kwa muda wa siku moja tu utapatwa na mapigo ya mauti, huzuni na njaa. Na zaidi ya hiyo utateketezwa kwa moto, kwa maana Bwana wetu, Mungu anayeuhukumu, ni mwenye uwezo.”

9Wafalme wa dunia waliozini nao na kujifurahisha pamoja nao wataulilia na kuufanyia kilio wakati watakapoona moshi wa moto utakaouteketeza ukipanda juu.

10Watasimama kwa mbali kwa ajili ya kuogopa yale mateso yake, wakisema: “Ole, ole kwako ewe muji Babeli, muji mukubwa na wenye uwezo! Kwa saa moja tu azabu yako imetimia!”

11Wachuuzi wa dunia watalia na kuufanyia kilio kwa sababu hakuna mutu atakayewanunulia tena biashara zao

12za zahabu, feza, mawe ya bei kali, ushanga, nguo zilizofumwa na nyuzi zuri pamoja na nguo nzuri za rangi nyekundu nyeusi na nyekundu sana, miti yote yenye kunuka vizuri, vyombo vyote vyenye kutengenezwa na pembe, na vyote vinavyochongwa na miti ya bei kali, na vyombo vyote vya shaba, vya chuma, vya mawe yenye kuchongwa,

13mudalasini, vitu vyote vya kufukiza, marasi, ubani, divai, mafuta, unga nzuri, ngano, ngombe, kondoo, farasi, magari, watumwa na hata roho za watu.

14Nao wale wachuuzi wanauambia muji ule: “Mazao mbalimbali uliyotamani sana kupata, yametoweka kwako. Na vitu vyote vya bei kali na vizuri vyenye kungaa vimekupotea, wala hautaviona tena.”

15Wachuuzi waliojitajirisha na biashara za muji ule, watasimama kwa mbali kwa ajili ya woga kwa kuona mateso yatakayoupata. Watalia na kufanya kilio,

16wakisema: “Ole! Ole kwa muji ule mukubwa. Ulikuwa unavaa nguo zilizofumwa na nyuzi nzuri pamoja na nguo zuri ya rangi nyekundu nyeusi na nyekundu sana. Ulikuwa unapambwa kwa zahabu, mawe ya bei kali, na ushanga wa bei kali!

17Kwa muda wa saa moja tu utajiri mwingi kama huu umeharibishwa.”

Waongozi wote wa mashua na wasafiri wao, nao wote wanaofanya kazi ndani ya mashua na wote wanaochuuza kwa njia ya bahari walisimama kwa mbali.

18Walilalamika walipoona moshi wa moto uliouteketeza ukipanda juu wakisema: “Muji gani ungeweza kulinganishwa na muji huu mukubwa!”

19Wakajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao, wakalia na kufanya kilio, nao walilalamika, wakisema: “Ole! Ole kwa muji ule mukubwa! Wote wanaokuwa na mashua za kufanya uchuuzi juu ya bahari walijitajirisha na mali zake nyingi. Lakini kwa muda wa saa moja tu umebaki mutupu.”

20Enyi mbingu, nanyi watu wa Mungu pamoja na mitume na manabii wake, mufurahi kwa ajili ya mambo yaliyotokea muji ule, kwa maana Mungu amewapatia haki yenu kwa kuuhukumu!

21Kisha malaika mumoja mwenye uwezo akanyanyua jiwe linalokuwa kama jiwe kubwa la kusagia. Akalitupa katika bahari akisema: “Ni hivi muji mukubwa wa Babeli utakavyotupwa kwa nguvu, nao hautaonekana tena.

22Sauti ya wapiga vinubi na ya wapiga vinanda, ya wapiga filimbi na ya baragumu, haitasikilika ndani yako tena. Fundi wa kazi yoyote hataonekana ndani yako tena hata kidogo wala kelele la jiwe la kusagia halitasikilika.

23Mwangaza wa taa hautaonekana tena ndani yako. Na hakutasikilika tena kelele la wenye kuoa au kuolewa. Itakutokea vile kwa sababu wachuuzi wako walikuwa wenye uwezo mukubwa katika dunia, nawe umewadanganya watu wote kwa njia ya vitendo vyako vya uchawi.”

24Muji Babeli umeazibiwa kwa sababu ndani yake kumeonekana damu ya manabii na ya watu wa Mungu pamoja na damu ya watu wote waliouawa katika dunia.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help