Matendo ya Mitume 22 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1“Wandugu zangu na wababa zangu, musikilize yale ninayotaka kusema kwa kujitetea mbele yenu.”

2Walipomusikia akisema nao katika luga ya Kiebrania, wakanyamaza zaidi. Halafu Paulo akasema:

3“Mimi ni Muyuda, nimezaliwa Tarso, katika jimbo la Kilikia, lakini nililelewa katika muji huu wa Yerusalema. Mimi nilikuwa mwanafunzi wa Gamalieli, na alinifundisha namna ya kufuata kabisa Sheria ya babu zetu. Nikajitolea kabisa kwa kutumikia Mungu kama vile ninyi wote munavyofanya leo.

4Mimi niliwatesa hata kuwaua watu waliofuata Njia ya Bwana. Niliwakamata wanaume na wanawake na kuwatupa katika kifungo.

5Hata Kuhani Mukubwa pamoja na baraza lote la wasimamizi wa watu wanaweza kushuhudia kwamba ninasema kweli. Nilipata hata barua toka kwao iliyoandikwa kwa ajili ya wandugu Wayuda wa Damasiki. Nikaenda kule kusudi niwafunge waamini waliokuwa kule na kuwaleta mpaka Yerusalema wapate kuazibiwa.

Paulo anaeleza jinsi alivyomugeukia Yesu(Mdo 9.1-19; 26.12-18)

6“Nilipokuwa katika safari karibu kufika Damasiki, yapata saa sita ya muchana, kwa rafla mwangaza mukubwa toka mbinguni ukanizunguka.

7Nikaanguka chini, nikasikia sauti ikiniambia: ‘Saulo, Saulo, kwa sababu gani unanitesa?’

8Nami nikauliza: ‘Wewe ni nani, Bwana?’ Na Bwana akanijibu: ‘Mimi ni Yesu wa Nazareti unayemutesa.’

9Watu waliokuwa pamoja nami wakaona mwangaza ule, lakini hawakusikia sauti ya yule aliyekuwa akinisemesha.

10Nikauliza: ‘Bwana, nifanye nini?’ Naye Bwana akanijibu: ‘Simama, uende Damasiki, na kule watakuambia mambo yote Mungu anayokuagiza kufanya.’

11Na kwa kuwa nilikuwa sioni tena kwa sababu ya ukali wa ule mwangaza, wenzangu wakanishika mukono na kuniongoza mpaka nikafika Damasiki.

12“Kule Damasiki kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Anania, mutu aliyeogopa Mungu na mwenye kushika Sheria yetu. Aliheshimiwa sana na Wayuda wote waliokaa kule.

13Yeye akanifikia, akasimama karibu nami na kuniambia: ‘Ndugu yangu Saulo, upate kuona tena!’ Na saa ile ile nikapata kuona na kuweza kumwona.

14Kisha akasema: ‘Mungu wa babu zetu amekwisha kukuchagua wewe kusudi ujue mapenzi yake. Anataka umwone Mwenye Haki, na kumusikia akisema kwa kinywa chake mwenyewe.

15Kwa maana utatoa ushuhuda wake kwa watu wote, utasema juu ya mambo yale uliyoona na kuyasikia.

16Basi sasa, unangojea nini? Simama ubatizwe na kuondolewa zambi zako, ukiomba kwa jina la Bwana.’ ”

Paulo anaeleza namna alivyotumwa kwa watu wa mataifa

17“Nilipokuwa nimekwisha kurudia Yerusalema, na nilipokuwa nikiomba katika hekalu, nikapata maono.

18Nikamwona Bwana, naye akaniambia: ‘Fanya haraka uondoke upesi katika muji huu Yerusalema kwa sababu watu wake hawatakubali ushuhuda utakaoutoa juu yangu.’

19Nami nikajibu: ‘Bwana, watu hawa wanajua wazi kwamba nilikuwa nikipitapita katika nyumba za kuabudia kwa kuwafunga na kuwapiga wale wanaokuamini.

20Na wakati watu walipomwua Stefano, aliyetoa ushuhuda juu yako, mimi mwenyewe nilikuwa pale, nami nilikuwa nimekubaliana nao juu ya kuuawa kwake. Na zaidi ya ile ni mimi niliyechunga nguo za wale waliomwua.’

21Halafu Bwana akaniambia: ‘Kwenda, kwa maana nitakutuma mbali kwa watu wa mataifa mengine.’ ”

Paulo na mukubwa wa waaskari

22Makutano walimusikiliza Paulo mpaka aliposema maneno yale. Kisha wakasema kwa nguvu: “Mumuteketeze mutu huyu! Mumwue, kwa maana hastahili kuishi!”

23Wakalalamika sana, wakatupatupa nguo zao na kurusha mavumbi juu.

24Yule mukubwa wa jeshi akaamuru waaskari wamupeleke Paulo katika upango wao. Akaamuru vilevile wamupige fimbo, kusudi apate kujua sababu gani watu walilalamika vile kwa ajili yake.

25Lakini walipokwisha kumufunga Paulo na kamba kusudi wamupige, yeye akamwambia jemadari mumoja aliyekuwa pale: “Sheria inawaruhusu kumupiga mwanainchi wa Roma, ingawa hajahukumiwa bado?”

26Yule jemadari aliposikia maneno hayo akaenda kwa yule mukubwa wa jeshi kwa kumupasha na kumwuliza: “Unataka kufanya nini? Mutu huyu ni mwanainchi wa Roma!”

27Basi jemadari akamwendea Paulo kumwuliza: “Uniambie ukweli, wewe ni mwanainchi wa Roma?”

Paulo akamujibu: “Ndiyo.”

28Halafu mukubwa wa jeshi akasema: “Mimi nilinunua haki ya kuwa mwanainchi wa Roma kwa feza nyingi.”

Paulo akamwambia: “Mimi ni mwanainchi wa Roma kwa kuzaliwa.”

29Mara moja wale waliotaka kumusambisha kwa kumupiga fimbo wakamwacha. Yule mukubwa wa jeshi akaogopa alipotambua kwamba Paulo ni mwanainchi wa Roma, na kwamba alikuwa anamufunga na minyororo.

Paulo mbele ya Baraza Kubwa

30Kesho yake, jemadari alitaka kujua mashitaki kamili ya Wayuda juu ya Paulo. Kwa hiyo akamufungua na kuamuru wakubwa wa makuhani pamoja na Baraza Kubwa wafanye mukutano. Kisha akamuleta Paulo na kumusimamisha mbele yao.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help