Hesabu 25 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Waisraeli na Bali wa Peori

1Waisraeli walipokuwa kule Sitimu, wanaume wakaanza kuzini na wanawake wa Moabu.

2Wanawake hao waliwaalika Waisraeli washiriki matambiko waliyotambikia miungu yao, nao Waisraeli wakakula chakula na kuabudu miungu yao.

3Ndivyo Waisraeli walivyojiunga na mungu Bali wa Peori, nayo hasira ya Yawe ikawaka juu yao.

4Basi, Yawe akamwambia Musa: Utwae viongozi wote wa Israeli, uwatundike mbele yangu jua kati, kusudi kasirani yangu juu yenu ipite.

5Musa akawaambia waamuzi wa Israeli: Kila mumoja wenu amwue mutu yeyote kati yenu ambaye amejiunga na mungu Bali wa Peori.

6Wakati huohuo mutu mumoja akamuleta mwanamuke mumoja Mumidiani katika nyumba yake, Musa na Waisraeli wote pamoja wakiwa wanaomboleza kwenye mulango wa hema la mukutano.

7Basi, Finehasi mwana wa Eleazari mujukuu wa kuhani Haruni alipoona hayo, akasimama, akatoka, akatwaa mukuki

8na kumufuatilia yule Mwisraeli mpaka ndani ya hema, akawachoma mukuki wote wawili ndani ya tumbo. Ugonjwa mukali uliokuwa umewaangamiza Waisraeli ukakomeshwa.

9Waliokufa kutokana na ugonjwa ule mukali walikuwa watu elfu makumi mbili na ine.

10Yawe akamwambia Musa:

11Finehasi mwana wa Eleazari, mujukuu wa kuhani Haruni, ameizuia hasira yangu juu ya Waisraeli; kati yenu ni yeye tu aliyeona wivu kama ule ninaokuwa nao mimi. Ndiyo maana sikuwaangamiza Waisraeli wote kwa hasira yangu.

12Kwa hiyo umwambie kwamba ninafanya naye agano la amani.

13Ninaagana naye kwamba yeye na wazao wake watakuwa makuhani milele kwa sababu aliona wivu kwa ajili yangu mimi Mungu wake, akawafanyia Waisraeli upatanisho.

14Huyo Mwisraeli aliyeuawa pamoja na mwanamuke wa Kimidiani aliitwa Zimuri mwana wa Salu, kiongozi wa jamaa moja katika kabila la Simeoni.

15Na huyo mwanamuke Mumidiani aliyeuawa aliitwa Kozibi binti ya Suri, aliyekuwa kiongozi wa ukoo fulani huko Midiani.

16Yawe akamwambia Musa:

17Uwachokoze Wamidiani na kuwaangamiza,

18kwa sababu waliwachokoza ninyi kwa werevu wao, ambao kwa njia yake wamewadanganya katika jambo la Peori, na kwa sababu ya Kozibi, binti yao, aliyeuawa wakati ugonjwa mukali ulipotokea kule Peori.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help