1Wandugu, si lazima kwenu niwaandikie jambo lolote juu ya wakati wala saa ambayo mambo hayo yatatokea.
2Kwa maana munajua ninyi wenyewe kwamba siku Bwana atakaporudia, itatimia kwa saa musiyozania kama vile mwizi anavyokuja usiku.
3Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.
4Lakini ninyi wandugu, hamuko katika giza, kwa hiyo siku ile haitawafikia kwa rafla kama mwizi.
5Kwa maana ninyi wote ni watu wanaoishi katika mwangaza, ndio watu wa muchana. Sisi si watu wa usiku wala wa giza.
6Basi tusilale usingizi kama vile wengine, lakini tukeshe na kuwa wakadirifu.
7Kwa maana wale wanaolala usingizi wanalala usiku, na wale wanaolewa, wanalewa usiku.
8Lakini sisi ni watu wa muchana, tunapaswa kuwa wakadirifu. Tunapaswa kushikamana na imani na upendo kama vile nguo ya chuma ya kukingia kifua, nalo tumaini letu la wokovu kama vile kofia ya kutulinda.
9Kwa maana Mungu hakututayarishia kuangamizwa kwa ukali wa kasirani yake, lakini kuokolewa kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
10Yeye alikufa kwa ajili yetu, kusudi hata ikiwa tuko wazima au tumekufa, tupate kuishi pamoja naye wakati atakaporudia.
11Basi mufarijiane na kujengana imani, kama vile munavyozoea kufanya.
Maonyo na salamu za mwisho12Wandugu, tunawaomba muwaheshimu sana wale wanaoshugulika na kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwaonya.
13Muwape heshima kubwa na kuwapenda kwa ajili ya kazi yao. Mukuwe na amani kati yenu.
14Tunawasihi wandugu, muwaonye wale wanaokuwa wavivu, muwatie moyo wale wanaoregea, muwasaidie wale wanaokuwa zaifu, na mukuwe wavumilivu kwa watu wote.
15Muangalie vema, hata mumoja wenu asimurudishie mwenzake ubaya kwa ubaya, lakini mutafutiane wema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.
16Mukuwe na furaha siku zote.
17Muombe bila kuchoka.
18Mumushukuru Mungu katika mambo yote. Kwa maana hayo ndiyo mambo Mungu anayotaka mufanye katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.
19Musizuize kazi ya Roho Mutakatifu.
20Musizarau ujumbe unaotoka kwa Mungu.
21Lakini muchunguze kila jambo na kushika lile linalokuwa jema.
22Muepuke ubaya wa kila namna.
23Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa, alinde uzima wenu wote ndiyo roho, moyo na mwili wenu, kusudi visikutiwe na kosa wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakaporudia.
24Yule anayewaita ninyi atatimiza mambo hayo, kwa maana yeye ni mwaminifu.
25Wandugu, mutuombee vilevile.
26Musalimiane kwa upendo wa kikristo.
27Ninawasihi kwa jina la Bwana, musome barua hii kwa wandugu wote.
28Tunawatakia neema kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.