1Yesu alianza kufundisha tena pembeni ya ziwa la Galilaya. Kundi kubwa la watu walikusanyika karibu naye, kwa hiyo akaingia ndani ya chombo na kuikaa mule. Chombo kilikuwa katika ziwa na watu walisimama inchi kavu, pembeni ya ziwa.
2Yesu akawafundisha mambo mengi akitumia mifano. Yeye akawaambia hivi katika mafundisho yake:
3“Musikilize! Mutu mumoja alikwenda kupanda mbegu.
4Alipokuwa akipanda mbegu katika shamba, zimoja zikaanguka pembeni ya njia, nao ndege wakakuja na kuzikula.
5Zingine zikaanguka pahali penye mawe pasipokuwa udongo mwingi. Mbegu zile zikaota upesi kwa sababu hapakukuwa udongo mwingi.
6Wakati jua lilipokuwa kali, likazichoma, na kwa sababu hazikukuwa na mizizi mikubwa zikakauka.
7Mbegu zingine zilianguka katikati ya miiba. Ile miiba ikaota na kuzisonga mbegu hata hazikuweza kutoa kitu.
8Lakini mbegu zingine zikaanguka katika udongo muzuri, mimea ikaota, ikakomaa na kuzaa matunda: zimoja zikazaa punje makumi tatu, zingine makumi sita na zingine punje mia moja.”
9Kisha akawaambia: “Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!”
Kusudi la kutumia mifano(Mat 13.10-17; Lk 8.9-10)10Wanafunzi kumi na wawili wa Yesu pamoja na watu waliokuwa pembeni yake walipokuwa peke yao, wakamwuliza awaelezee maana ya mifano ile.
11Yesu akawajibu: “Ninyi mumefunuliwa kujua siri ya Ufalme wa Mungu, lakini watu wengine wanaokuwa inje ya kikundi chenu wanasikia mambo yote kwa njia ya mifano,
12kusudi
‘Wapate kuangalia,
lakini wasione;
nao wapate kusikia,
lakini wasikuwe na ufahamu,
kusudi wasipate kumugeukia Mungu
na kusamehewa.’ ”
Yesu anaeleza mufano wa mupandaji(Mat 13.18-23; Lk 8.11-15)13Yesu akaongeza kuwaambia: “Kama musipoelewa mufano huu, namna gani mutaelewa mifano mingine?
14Mupandaji anapanda Neno la Mungu.
15Nafasi ile mbegu zilipoanguka pembeni ya njia, ni mufano wa watu wanaosikia Neno la Mungu, lakini mara moja Shetani anakuja na kuondoa lile Neno lililopandwa ndani yao.
16Udongo wenye mawe, pahali mbegu zilipoanguka ni mufano wa watu wanaosikia Neno la Mungu, na mara moja wanalipokea kwa furaha.
17Lakini halizami ndani yao kama mizizi; wanalishika kwa muda mufupi tu. Wakati taabu na mateso vinapowafikia kwa ajili ya Neno la Mungu, mara moja wanaanguka.
18Udongo wenye miiba, pahali mbegu zilipoanguka, ni mufano wa wale wanaosikia Neno la Mungu,
19lakini masumbuko ya dunia hii, udanganyifu wa mali, na tamaa za namna nyingine vikiwaingia, vinasonga lile Neno linalokuwa ndani yao na kulizuiza kuzaa matunda.
20Nao udongo muzuri, walimopanda mbegu, ni mufano wa watu wanaosikia Neno la Mungu na kulipokea. Nao wanazaa matunda; wamoja matunda makumi tatu, wengine makumi sita na wengine mia moja.”
Mufano wa tua(Lk 8.16-18)21Kisha Yesu akawaambia: “Taa inaletwa kwa kufunikiwa chini ya kitunga au chini ya kitanda? Si wanaiweka juu ya kinara?
22Ni hivi vilevile hakuna chochote kinachofichwa kitakachokosa kuonekana wazi, wala hakuna siri itakayokosa kufunuliwa waziwazi.
23Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!”
24Yesu akawaambia tena: “Muangalie vizuri maneno munayosikia! Mungu atawapimia na kipimo kile munachowapimia wengine, na kuwaongezea hata zaidi.
25Kwa maana anayekuwa na kitu, ataongezewa kingine; lakini asiyekuwa na kitu, ataondolewa hata kidogo anachokuwa nacho.”
Mufano wa mbegu zinazoota zenyewe26Yesu akaendelea kusema: “Ufalme wa Mungu unafanana na mutu mumoja aliyepanda mbegu katika shamba lake.
27Kila siku alilala na kuamuka na mbegu ziliota na kukomaa. Lakini hakujua namna gani mbegu zilivyoota.
28Udongo wenyewe unaotesha mimea; kwanza majani, halafu masuke na kisha ngano zinazokomaa ndani ya masuke.
29Wakati ngano zinapokomaa, mutu anazivuna, kwa maana ni wakati wa mavuno.”
Mufano wa mbegu ndogo sana ya haradali(Mat 13.31-32,34; Lk 13.18-19)30Yesu akasema tena: “Tufananishe Ufalme wa Mungu na nini? Au tuulinganishe na mufano gani?
31Unafanana na mbegu ya haradali. Inapopandwa katika udongo ni ndogo sana kuliko mbegu zote za dunia.
32Lakini ikiisha kupandwa, inaota na kuwa kubwa zaidi kuliko mimea yote. Inatoa matawi makubwa hata ndege wanaweza kujenga chicha zao juu yake, kwenye kivuli chake.”
33Yesu aliwafundisha watu kwa mifano mingi ya namna hii kwa kadiri walivyoweza kuelewa.
34Hakusema nao pasipo kutumia mifano lakini alipokuwa pamoja na wanafunzi wake peke yao, aliwafasiria mambo yote.
Yesu anatuliza zoruba(Mat 8.23-27; Lk 8.22-25)35Na ilipotimia magaribi siku ile ile, Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Tuvuke ngambo ingine ya ziwa.”
36Basi wanafunzi wakaaga kundi la watu, wakaingia ndani ya chombo Yesu alimokuwa na kuondoka pamoja naye. Na vyombo vingine vikamusindikiza.
37Zoruba kali ikavuma ndani ya ziwa, maji yakajitupatupa ndani ya chombo hata kikaanza kujaa.
38Yesu alikuwa upande wa nyuma wa chombo, akilala usingizi akilalisha kichwa juu ya mufuko wa kuegemea. Wanafunzi wake wakamwamusha na kumwambia: “Mwalimu, haikuhangaishi kuona sisi tunakufa?”
39Yesu akaamuka, akakaripia ile zoruba na kuiambia ziwa: “Kimya! Tulizana!”
Basi zoruba ikakoma na kukakuwa kimya kabisa.
40Kisha Yesu akawaambia wanafunzi: “Sababu gani munaogopa? Mpaka sasa hamujakuwa na imani?”
41Halafu wakaogopa sana, nao wakaanza kuulizana: “Huyu ni mutu gani, hata zoruba na ziwa vinamutii?”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.