Isaya 26 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Wimbo wa ushindi

1Siku ile watu wataimba wimbo huu katika inchi ya Yuda:

Sisi tuna muji imara:

Mungu anatulinda kwa kuta na upango.

2Mufungue milango ya muji,

taifa aminifu liingie;

taifa linalotenda mambo ya haki.

3Ee Mungu, unawaweka katika amani wanaokuwa imara,

unawaweka katika amani kwa sababu wanakutegemea.

4Mutumainie Yawe siku zote

kwa maana yeye ni kikingio chetu kwa milele.

5Amewaporomosha waliokaa pande za juu,

muji wenye utukufu ameuangusha mpaka chini,

ameutupa mpaka katika mavumbi.

6Sasa muji huo unakanyagwakanyagwa

kwa miguu ya watu wamasikini na wazaifu.

7Njia ya watu wa haki ni yenye kunyooka;

ewe Mungu mwenye haki, unasawanisha njia yao.

8Katika njia ya maamuzi yako

tunakungojea ee Yawe;

tamaa yetu ni kulikumbuka jina lako.

9Moyo wangu unakutamani usiku kucha,

nafsi yangu inakutafuta kwa moyo.

Utakapohukumu dunia,

watu wote katika ulimwengu watajifunza haki.

10Lakini waovu hata wakipewa rehema,

hawawezi kujifunza kutenda haki.

Hata katika inchi ya usawa,

wao bado wanatenda maovu,

wala hawajali ukubwa wako wewe Yawe.

11Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu,

lakini hawauoni.

Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya.

Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!

12Wewe, ee Yawe, umetupatia amani;

umefanikisha shuguli zetu zote.

13Ee Yawe, Mungu wetu,

tulipata kutawaliwa na wabwana wengine ambao si wewe,

lakini tunakubali wewe pekee kuwa Mungu wetu.

14Watu hao wamekufa, wala hawataishi tena;

wamekuwa mizimu, wala hawatafufuka.

Maana wewe umewaazibu na kuwaangamiza,

hakuna atakayeweza kuwakumbuka tena.

15Umezidisha taifa letu, ee Yawe,

umelizidisha taifa letu.

Umeipanua mipaka yote ya inchi,

kwa hiyo wewe unatukuzwa.

16Ee Yawe, walipotaabika walikutafuta,

walikuomba musaada ulipowaazibu.

17Kama vile mama mwenye mimba anayezaa

analia na kugaagaa kwa uchungu,

ndivyo tulivyokuwa kwa sababu yako, ee Yawe.

18Sisi tulipata maumivu ya kuzaa,

lakini tukazaa tu upepo!

Hatukupata ushindi wowote kwa ajili ya inchi yetu,

hatukuweza kuongeza hesabu ya watu katika inchi.

19Wafu wako wataishi tena,

miili yao itafufuka.

Wanaolala katika mavumbi wataamuka na kuimba kwa furaha!

Mungu atapeleka umande wake wa uzima,

nao wanaokuwa kwa wafu watatoka wazima. Kisha azabu ni faraja

20Mukuje watu wangu, muingie ndani ya nyumba zenu,

mujifungie humo ndani.

Mujifiche kwa muda mufupi,

mpaka kasirani ya Yawe ipite.

21Maana Yawe anakuja kutoka kwake juu,

kutoka makao yake huko mbinguni;

kuwaazibu wakaaji wa dunia kwa uovu wao.

Nayo dunia haitaficha tena wale waliouawa,

lakini itaufichua umwagaji wa damu wote.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help