Kumbukumbu la Sheria 1 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Utangulizi

1Kitabu hiki kina maneno ambayo Musa aliwaambia watu wote wa Israeli wakati walipokuwa katika jangwa upande wa mashariki wa muto Yordani. Walikuwa katika bonde la Yordani karibu na Sufu, kati ya muji wa Parani upande mumoja na miji ya Tofeli, Labani, Hazeroti na Dizahabu upande mwingine.

2(Ni mwendo wa siku kumi na moja kutoka mulima Horebu mpaka Kadesi-Barnea kwa njia ya mulima Seiri.)

3Siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na moja, mwaka wa makumi ine nyuma ya kutoka Misri, Musa akawaambia watu kila kitu ambacho Yawe alimwamuru awaambie.

4Alifanya hivyo kisha Yawe kumushinda mufalme Sihoni wa Waamori ambaye alikuwa anakaa katika muji wa Hesiboni, na mufalme Ogi wa Basani ambaye alikuwa anakaa katika muji wa Astaroti na Edirei.

29“Lakini mimi nikawaambia hivi: ‘Musikuwe na hofu wala musiwaogope watu hao.’

30Yawe, Mungu wenu, ambaye anawatangulia, yeye mwenyewe atapigana kwa ajili yenu kama vile alivyofanya mbele yenu kule Misri na

31kule katika jangwa ambako muliona jinsi alivyowabeba safari hiyo yote kama vile baba anavyobeba mwana wake, mpaka mukafika hapa.

32Lakini ingawa nilisema hayo yote, ninyi hamukumwamini Yawe, Mungu wenu,

33ambaye aliwatangulia katika njia na kuwatafutia pahali pa kupiga kambi zenu. Usiku aliwatangulia kwa moto na muchana kwa wingu, kwa kuwaonyesha njia.

34“Yawe akasikia manunguniko yenu, akakasirika, akaapa akisema:

35‘Hakuna hata mumoja wenu katika kizazi hiki kiovu atakayeingia katika ile inchi nzuri niliyoahidi kuwapa wazee wenu.

36Kalebu mwana wa Yefune, ndiye tu atakayeiona. Nami nitamupatia inchi hiyo aliyokanyaga ndani ikuwe yake yeye na wazao wake kwa sababu amekuwa mwaminifu kabisa kwangu.’

37Yawe akanikasirikia mimi vilevile kwa sababu yenu, akasema: ‘Hata wewe Musa hautaingia katika inchi hiyo.

38Lakini musaidizi wako Yoshua mwana wa Nuni ataingia humo. Basi, umutie moyo maana yeye atawaongoza watu wa Israeli wairizi inchi hiyo’.

39Kisha Yawe akatuambia sisi wote: ‘Hao watoto wenu munaoogopa kwamba watakuwa mateka za waadui zenu, hakika hao wanaokuwa wadogo ambao hawajui bado kupambanua kati ya mazuri na mabaya, hao ndio watakaoingia huko, nami nitawapa wao inchi hiyo ikuwe yao.

40Lakini ninyi, mugeuke na kurudi katika jangwa kuelekea bahari Nyekundu.’

41“Kisha mukanijibu: ‘Sisi tumemutendea Yawe zambi, lakini sasa tutakwenda na kupigana kama vile Yawe, Mungu wetu alivyotuamuru’. Hivyo, kila mumoja wenu akajitayarisha kupigana vita, maana mulifikiri kwamba lingekuwa jambo jepesi kuishambulia inchi hiyo ya milima.

42Naye Yawe akaniambia: ‘Uwaambie hao watu wasiende kupigana kwa sababu siko pamoja nao. Wasiende, kusudi wasishindwe na waadui zao’.

43Basi, mimi nikawaambia hivyo, lakini ninyi hamukusikia. Pahali pake mukakataa kufuata agizo la Yawe. Bila kujali mukaingia katika inchi hiyo ya milima.

44Hapo, Waamori waliokuwa wanaishi katika eneo hilo la milima wakateremuka kuwashambulia na kama vile nyuki wanavyofanya wakawapiga huko Seiri mpaka Horma.

45Ndipo muliporudi, mukamulilia Yawe, lakini hakuwasikiliza wala hakuwajali.

46Basi, mukabaki kule Kadesi kwa muda murefu ambao mulikaa kule.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help