1Yawe akamwambia Musa:
2Uwaambie Waisraeli kwamba mutakapofika katika inchi ninayowapa ambamo mutaishi,
3mukinitolea mimi Yawe sadaka kutoka katika mifugo yenu, sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kutimiza kiapo au kutoa sadaka ya mapenzi au sadaka ya wakati wa sikukuu zenu zilizowekwa, na kufanya harufu nzuri ya kunipendeza mimi Yawe,
4basi, yule anayetoa sadaka yake, atamuletea vilevile Yawe sadaka ya vyakula ya kilo moja ya unga laini uliopondwa na kuchanganywa na litre moja ya mafuta.
5Toa litre moja ya divai kama sadaka ya kinywaji kwa kila mwana-kondoo wa sadaka ya kuteketezwa kwa moto au sadaka ingine.
6Wakati wa kutoa sadaka ya kondoo dume, kilo mbili za unga uliopondwa na litre moja na nusu ya mafuta vitatolewa kama sadaka ya vyakula,
7pamoja na sadaka ya kinywaji ya litre moja na nusu ya divai, na kufanya harufu nzuri ya sadaka ya kumupendeza Yawe.
8Wakati mutakapomutolea Yawe mwana-ngombe dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au sadaka kwa kutimiza kiapo au kwa ajili ya sadaka za amani,
9mutu atamutoa kama vile sadaka pamoja na sadaka ya vyakula ya unga wa kilo tatu unaokuwa muzuri na litre mbili za mafuta,
10pamoja na sadaka ya kinywaji ya litre mbili za divai, na kufanya harufu nzuri ya sadaka ya kumupendeza Yawe.
11Hivi ndivyo vitu vitakavyotolewa pamoja na kila mwana-ngombe dume, kondoo dume au mbuzi.
12Hesabu ya vitu hivyo itaongezwa kulingana na hesabu ya nyama watakaotolewa.
13Kila mwananchi Mwisraeli atafuata maagizo hayo wakati anapotoa sadaka, harufu inayomupendeza Yawe.
14Na kama kuna mugeni anayeishi pamoja nanyi kwa muda au siku zote, akitaka kutoa sadaka yake kwa kuiteketeza kwa moto, harufu inayomupendeza Yawe, mutu huyo atafanya kama vile munavyofanya ninyi.
15Katika vizazi vyote vinavyokuja, masharti yaleyale mutakayofuata ninyi ndiyo mugeni yeyote atakayeishi pamoja nanyi atakayofuata; mbele ya Yawe mutakuwa sawa.
16Ninyi na yeye mutakuwa chini ya sheria ileile moja na maagizo yaleyale.
17Yawe akamwambia Musa: Uwaambie
18Waisraeli kwamba wakati watakapoingia katika inchi ninayowapeleka ndani yake
19kila mara mutakapokula mazao ya inchi hiyo, mutatenga sehemu fulani na kunipa mimi Yawe.
20Mutakapopika mukate, mukate wa kwanza wa mazao ya kwanza ya ngano yenu utatolewa kama sadaka kutoka pahali pa kupepetea ngano.
21Mutanitolea mimi Yawe sadaka hii katika vizazi vyenu vyote vinavyokuja.
22Lakini kama mutakosa kufuata amri zote ambazo mimi Yawe nimewapa kwa njia ya Musa,
23kama siku zinazokuja watu hawatafuata yote ambayo mimi Yawe nimemwamuru Musa,
24basi, ikiwa kosa hilo limefanyika bila kukusudia, bila Waisraeli wote pamoja kujua, watatoa mwana-ngombe dume mumoja kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumupendeza Yawe, pamoja na sadaka yake ya vyakula na ya kinywaji kufuatana na maagizo yake. Vilevile watu watatoa beberu mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi.
25Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya Waisraeli wote pamoja, nao watasamehewa kwa sababu si kosa lililokusudiwa, na wameleta sadaka yao, sadaka ya kuteketezwa kwa Yawe kama sadaka ya zambi kwa ajili ya kosa lao.
26Waisraeli wote, pamoja na wageni wanaoishi nao, watasamehewa kwa sababu wote walielekewa na kosa hilo.
27Mutu mumoja akifanya zambi bila kujua, atatoa mbuzi dike wa mwaka mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi. Ang. Law 4.27-31
28Kuhani atafanya upatanisho mbele ya Yawe, kwa ajili ya huyo mutu aliyekosa bila kujua, naye atasamehewa.
29Mutafuata sheria moja kila mutu atakayekosa bila kukusudia, akuwe ni mwanainchi Mwisraeli au ni mugeni anayeishi pamoja nanyi.
30Lakini mutu yeyote atakayekosa kwa makusudi, akuwe mwanainchi au mugeni, atakuwa amemutukana Yawe, na anapaswa kutengwa mbali kati ya watu wake.
31Maana amekataa neno la Yawe na kuvunja moja kati ya amri zake. Mutu huyo atatengwa mbali kabisa; na lazima ya kifo chake itakuwa juu yake mwenyewe.
Kuvunja Sabato32Siku moja, wakati Waisraeli walipokuwa katika jangwa, wakamwona mutu mumoja akiokota kuni siku ya Sabato.
33Basi, mutu huyo akapelekwa mbele ya Musa, Haruni na Waisraeli wengine wote.
34Wao wakamuweka katika kifungo kwa sababu haikukuwa bado imesemwa wazi namna ya kumufanya mutu wa namna hiyo.
35Halafu Yawe akamwambia Musa: Mutu huyo anapaswa kuuawa; Waisraeli wote pamoja watamupiga mawe inje ya kambi.
36Basi, watu wakamutoa inje ya kambi, wakamupiga mawe mpaka akakufa, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
Vishada katika incha za nguo37Kisha Yawe akamwambia Musa:
38Uwaambie watu wa Israeli, uwaagize wajifanyie vishada katika incha za nguo zao, na kutia nyuzi za rangi ya samawi juu ya kila kishada. Uwaambie wafanye hivyo katika vizazi vyao vyote vinavyokuja. Ang. Kumb 22.12
39Vishada hivyo vitakuwa ukumbusho kwenu. Kila mara mutakapoviona, mutakumbuka amri zangu zote na kuzifuata, kusudi musifuate mapenzi yenu na yale munayoona kwa macho yenu wenyewe.
40Vishada hivyo vitawakumbusha amri zangu zote na mutazifuata zote kwa ukamilifu, nanyi mutakuwa watakatifu wangu.
41Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri kusudi nikuwe Mungu wenu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.