Mwanzo 46 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Yakobo anakwenda Misri

1Basi, Israeli akaanza safari yake pamoja na mali yake yote. Alipofika Beri-Seba, akatoa sadaka kwa Mungu wa baba yake Isaka.

2Mungu akaongea na Israeli katika maono usiku, akamwita: “Yakobo! Yakobo!”

Yakobo akaitika: “Niko hapa.”

3Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu, Mungu wa baba yako. Usiogope kwenda Misri. Utakapokuwa kule, nitakufanya kuwa taifa kubwa.

4Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nawe kule Misri na kukurudisha huku. Utakapokufa, mukono wa Yosefu ndio utakaofumba macho yako.”

5Basi, Yakobo akaondoka Beri-Seba. Wana wake wakamupeleka yeye, watoto wao wachanga pamoja na wake zao katika magari ambayo mufalme wa Misri alituma kwa kumubeba.

6Walipeleka vilevile nyama na mali yao yote waliyokuwa wamechuma katika inchi ya Kanana, wakakwenda Misri. Yakobo aliwapeleka wazao wake wote:

7wana wake, wajukuu wake wanaume na wanawake. Wote akawaleta Misri.

8Hawa ndio wazao wa Israeli ambao walikwenda Misri pamoja naye:

Rubeni, muzaliwa wake wa kwanza,

9pamoja na wana wa Rubeni: Hanoki, Palu, Hesironi na Karmi.

10Simeoni na wana wake: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Sauli, aliyezaliwa kwa mwanamuke Mukanana.

11Lawi na wana wake: Gersoni, Kohati na Merari.

12Yuda na wana wake: Eri, Onani, Sela, Peresi na Zera. (Lakini Eri na Onani walikufa katika inchi ya Kanana). Wana wa Peresi walikuwa Hesironi na Hamuli.

13Isakari na wana wake: Tola, Puwa, Yasubu na Simuroni.

14Zebuluni na wana wake: Seredi, Eloni na Yaleli.

15Hao ndio wana ambao Lea alimuzalia Yakobo kule Padani-Aramu, pamoja na Dina binti yake. Jumla ya wana wake, wabinti zake na wajukuu wake walikuwa watu makumi tatu na watatu.

16Gadi na wana wake: Sifioni, Hagi, Suni, Esiboni, Eri, Arodi na Areli.

17Aseri na wana wake: Imuna, Isiwa, Isiwi, Beria na Sera, dada yao. Beria na wana wake: Heberi na Malkieli.

18Hawa kumi na sita ni wazao wa Yakobo na Zilpa, mujakazi ambaye Labani alimupa binti yake Lea.

19Rakeli alimuzalia Yakobo wana wawili: Yosefu na Benjamina.

20Kule Misri, Asenati binti ya Potifera, aliyekuwa kuhani wa muji wa Oni, alimuzalia Yosefu wana wawili: Manase na Efuraimu.

21Wana wa Benjamina walikuwa Bela, Bekeri, Asibeli, Gera, Namani, Ehi, Rosi, Mupimu, Hupimu na Ardi.

22Watu hao kumi na wane ni wazao wa Yakobo na muke wake Rakeli.

23Dani na mwana wake Husimu.

24Nafutali na wana wake: Yaseli, Guni, Yeseri na Silemu.

25Hao saba ni wazao wa Yakobo na Biliha, mujakazi ambaye Labani alimupa binti yake Rakeli.

26Jumla ya wazao wa Yakobo aliokwenda nao Misri, bila kuwahesabu wake za wana wake, ilikuwa watu makumi sita na sita.

27Kule katika inchi ya Misri Yosefu alikuwa amepata wana wawili. Kwa hiyo watu wote wa jamaa ya Yakobo walioingia Misri walikuwa makumi saba.

Yakobo anafika Misri

28Yakobo akamutanguliza Yuda kwa Yosefu kumwomba waonane kule Goseni. Nao wakafika katika eneo la Goseni.

29Yosefu akapanda gari lake la farasi, akakwenda kumupokea baba yake Israeli, kule Goseni. Alipomufikia baba yake, alimukumbatia na kulia kwa kitambo kirefu.

30Israeli akamwambia Yosefu: “Hata nikikufa sasa si kitu kwa sababu nimeuona uso wako na kujua kwamba wewe uko muzima!”

31Yosefu akawaambia wandugu zake na jamaa yote ya baba yake: “Ninakwenda kumwarifu mufalme wa Misri kwamba wandugu zangu na jamaa yote ya baba yangu waliokuwa katika inchi ya Kanana wamekuja kwangu.

32Nitamwelezea kwamba ninyi ni wachungaji maana mumekuwa mukichunga nyama, na kwamba mumefika pamoja na mbuzi, kondoo, ngombe na mali yenu yote.

33Basi, mufalme akiwaita na kuwauliza: ‘Kazi yenu ni nini?’

34Museme: ‘Bwana, sisi watumishi wako, ni wafugaji wa nyama tangu utoto wetu mpaka leo, maana ndivyo babu zetu walivyokuwa.’ Museme hivyo kusudi muruhusiwe kukaa katika eneo la Goseni.” Yosefu alisema hivyo kwa sababu kwa Wamisri wachungaji wote wa kondoo ni chukizo.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help