1Wimbo wa sifa wa Daudi.
Nitakutukuza, ee Mungu wangu na mufalme wangu;
nitalitukuza jina lako kwa milele na milele.
2Nitakutukuza kila siku;
nitalisifu jina lako kwa milele na milele.
3Yawe ni mukubwa, anastahili sifa nyingi;
ukubwa wake hauwezi kuchunguzika.
4Sifa za matendo yako zitaelezwa kwa kizazi hata kizazi,
watu watatangaza matendo yako makubwa.
5Nitasema juu ya utukufu na mamlaka yako,
nitafikiri juu ya matendo yako ya ajabu.
6Watu watatangaza ukubwa wa matendo yako ya ajabu,
nami nitatangaza ukubwa wako.
7Watatangaza sifa za uzuri wako mwingi,
na kuimba juu ya haki yako.
8Yawe ni mwenye huruma na rehema;
yeye hakasiriki upesi, amejaa wema.
9Yawe ni muzuri kwa wote,
ni mwenye huruma kwa viumbe vyake vyote.
10Viumbe vyako vyote vitakushukuru, ee Yawe,
nao waaminifu wako watakutukuza.
11Watasema juu ya utukufu wa ufalme wako,
na kutangaza juu ya nguvu yako kubwa,
12kusudi kila mutu ajue matendo yako makubwa,
na mamlaka ya ufalme wako wenye utukufu.
13Ufalme wako ni ufalme wa milele;
mamlaka yako yanadumu vizazi vyote.
Yawe ni mwaminifu katika ahadi zake zote,
ni mwema katika matendo yake yote.
14Yawe anawashikilia wote wanaoanguka;
anawainua wote waliogandamizwa.
15Viumbe vyote vinakutazamia,
nawe unavipatia chakula chao kwa wakati wake.
16Unafumbua mukono wako kwa moyo safi,
unatimiza mahitaji ya kila kiumbe kinachoishi.
17Yawe ni mwenye haki katika njia zake zote;
ni mwema katika matendo yake yote.
18Yawe yuko karibu na wote wanaomwomba,
wote wale wanaomwomba kwa uaminifu.
19Anajibia mahitaji yao wote wanaomwabudu;
anasikia kilio chao na kuwaokoa.
20Yawe anawalinda wote wanaomupenda;
lakini anawaangamiza waovu wote.
21Nitatangaza sifa za Yawe;
viumbe vyote vilisifu jina lake takatifu,
kwa milele na milele.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.