Isaya 37 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mufalme anaomba shauri kwa nabii Isaya(2 Fal 19.1-7)

1Mufalme Hezekia aliposikia habari hiyo, alipasua nguo yake, akavaa nguo ya gunia, akaingia katika nyumba ya Yawe.

2Aliwaamuru Eliakimu, musimamizi wa nyumba ya kifalme, Sebuna, katibu, na wazee wa makuhani, wamwendee nabii Isaya mwana wa Amozi, wakiwa wamevaa nguo za magunia.

3Nao wakamwambia Isaya: “Hezekia anasema hivi: Leo ni siku ya huzuni, ya kuazibiwa, na ya kuzarauliwa. Sisi tumekuwa kama mwanamuke anayetaka kuzaa mutoto, lakini hana nguvu ya kumuzaa.

4Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyoyasikia. Uwaombee watu wanaobaki.”

5Basi, hao watumishi wa mufalme Hezekia walipokwisha kufika kwa Isaya,

6aliwaambia: “Mumwambie bwana wenu kwamba Yawe anasema hivi: Usiogope kwa sababu ya maneno uliyoyasikia, ambayo watumishi wa mufalme wa Asuria wameyasema kwa kunitusi.

7Sikia, nitamufanya mufalme asikie uvumi, halafu atarudi katika inchi yake, na kule nitamufanya auawe kwa upanga.”

Waasuria wanaogopesha tena(2 Fal 19.8-19)

8Kisha yule jemadari aliposikia kwamba mufalme wa Asuria alikuwa ameondoka Lakisi, aliondoka na kumukuta akishambulia muji wa Libuna.

9Halafu mufalme alipata habari kwamba Tiraka mufalme wa Etiopia anakuja kupigana naye. Akatuma wajumbe kwa Hezekia, akisema:

10“Mumwambie Hezekia mufalme wa Yuda: Usikubali Mungu wako unayemutegemea akudanganye kwa kukuahidi kwamba Yerusalema hautatekwa na mufalme wa Asuria.

11Wewe umekwisha kusikia jinsi wafalme wa Asuria walivyotendea inchi nyingine na kuziangamiza kabisa. Unazani wewe utaokoka?

12Miungu ya mataifa iliokoa Gozani, Harani, Resefu na Waedeni waliokaa Terasari, mataifa ambayo babu zangu waliyaangamiza?

13Wako wapi wafalme wa Hamati, Arpadi, Sefarwaimu, Hena na Iva?”

14Mufalme Hezekia alipokea barua kutoka kwa wajumbe na kuisoma. Kisha akaenda na kuingia katika nyumba ya Yawe, akaiweka mbele ya Yawe.

15Halafu akamwomba Yawe akisema:

16“Ee Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, unayeikaa katika kiti cha kifalme juu ya makerubi, ni wewe tu unayekuwa Mungu, unayetawala falme zote za ulimwengu. Wewe uliumba dunia na mbingu.

17Ee, Yawe, fungua macho uone, tega sikio lako uyasikie matusi yote ambayo Saniharibu amepeleka na kukutukana wewe Mungu Mwenye Uzima.

18Ee Yawe, ni kweli kwamba wafalme wa Asuria wameangamiza mataifa yote na inchi zao.

19Walitupa miungu yao katika moto kwa sababu haikukuwa miungu ya kweli, lakini sanamu za miti na mawe zilizochongwa na mikono ya watu.

20Sasa, ee Yawe, Mungu wetu, utuokoe toka katika makucha ya Saniharibu, kusudi falme zote za dunia zijue kwamba ni wewe peke yako, ee Yawe, ambaye ni Mungu.”

Ukumbe wa Isaya kwa mufalme(2 Fal 19.20-37)

21Kisha Isaya mwana wa Amozi alituma ujumbe kwa Hezekia, akisema:

Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kwa sababu umeniomba juu ya Saniharibu mufalme wa Asuria,

22basi huu ndio ujumbe wa Yawe juu ya huyo mufalme:

Watu wa Sayuni wanakuzarau kabisa,

Watu wa Yerusalema wanakutikisia kichwa kwa kukuchekelea.

23Wewe umemutukana nani?

Umemutusi nani?

Umesubutu kumufokea nani kwa majivuno?

Ni Mungu, Mutakatifu wa Israeli!

24Umewatuma watumishi wako kumuchekelea Bwana wenu;

wewe umesema: Kwa magari yangu mengi ya vita,

nimefika juu kwenye vichwa vya milima,

mpaka kwenye vichwa vya milima ya Lebanoni.

Nimeangusha mierezi yake mirefu,

na misunobari mizurimizuri.

Nimevifikia vichwa vyake

na ndani ya pori zake kubwa.

25Nimechimba visima na kunywa maji yake,

na nilikausha vijito vya Misri

kwa miguu yangu.

26Haujasikia, ewe Saniharibu, kwamba

mimi Yawe nilipanga jambo hili tangu zamani?

Ninachotimiza sasa nilikipanga zamani.

Nilikuweka uifanye miji yenye kuzungukwa na kuta

kuwa lundo la mabomoko.

27Wakaaji wake wakiwa wameishiwa nguvu,

wametishika na kufazaika,

wamekuwa kama mimea ya shamba,

kama majani changa,

kama majani yanayoota juu ya paa,

yanayokauka mbele ya kukomaa.

28Lakini, ninakujua wewe Saniharibu;

ninajua wakati unaikaa, wakati unatoka, na wakati unaingia;

ninajua vilevile wakati kasirani yako inawaka juu yangu.

29Kwa vile umefanya mipango juu yangu

na nimesikia majivuno yako,

nitatia ndoana yangu ndani ya pua yako,

na lijamu yangu ndani ya kinywa chako.

Nitakurudisha katika njia ileile uliyokuja ndani yake.

30Na hiki ndicho kitakuwa kitambulisho kwako Hezekia: Mwaka huu na mwaka unaokuja mutakula kinachoota chenyewe bila kupandwa. Lakini katika mwaka wa tatu mutapanda na kuvuna mavuno; mutapanda mizabibu na kula matunda yake.

31Wale watakaobaki katika ukoo wa Yuda wataongezeka na kuwa wengi kama vile muti unavyotoa mizizi yake katika udongo na kuzaa matunda juu.

32Maana kutakuwa watu watakaobaki kule Yerusalema; kule kwenye mulima Sayuni kutakuwa watu wachache watakaobakia. Yawe wa majeshi amekusudia kukamilisha hayo.

33Yawe anasema hivi juu ya mufalme wa Asuria: Hataingia katika muji huu, wala kuupiga mushale, wala kuingia akishika ngao, wala hatalundika udongo kandokando yake apate kuubomoa.

34-35Atarudi kwa njia ileile aliyokuja nayo wala hataingia katika muji huu. Kweli, kwa ajili ya heshima yangu mimi na kwa ajili ya mutumishi wangu Daudi, nitaulinda na kuuokoa muji huu. –Ni ujumbe wa Yawe.

36Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.

37Kisha Saniharibu mufalme wa Asuria akaondoka, akaenda kwake, akakaa Ninawe.

38Siku moja, wakati Saniharibu alipokuwa akiabudu katika nyumba ya Nisiroki mungu wake, wana wake wawili, Adarameleki na Sarezeri, walimwua kwa upanga, halafu wakakimbilia katika inchi ya Ararati. Halafu mwana wake Esari-Hadoni akatawala kwa pahali pake.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help