1Siku hiyo, kutatokea chemichemi ya kutakasa zambi na uchafu wa wazao wa Daudi na wakaaji wote wa Yerusalema.
2Wakati ule, nitaondoa majina ya sanamu za miungu katika inchi, wala hayatakumbukwa tena. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.– Na wanaojidai kuwa manabii nitawaondoa kabisa pamoja na tamaa zao za kuabudu sanamu.
3Mutu yeyote akijidai kuwa nabii, baba na mama yake waliomuzaa watamwambia: “Unapaswa kufa maana unasema uongo kwa jina la Yawe.” Na wale wazazi wake watamuchoma kisu akiwa anatabiri.
4Siku hiyo, kila nabii atapata haya kwa ajili ya maono yake anapotabiri. Hawatavaa nguo za manyoya kwa kudanganya watu,
5lakini kila mumoja atasema: “Mimi si nabii. Mimi ni mulimaji tu; nimerizi mashamba tangu ujana wangu.”
6Na mutu akimwuliza mumoja wao: “Vidonda hivi unavyokuwa navyo kwenye mikono yako vimetoka wapi?” Yeye atajibu: “Vidonda hivi nilivipata katika nyumba ya warafiki zangu.”
7Yawe wa majeshi anasema hivi:
Amuka, ee upanga!
Simama umushambulie muchungaji wangu,
muchungaji anayenitumikia.
Umuue muchungaji na kondoo watawanyike.
Nitaunyoosha mukono wangu
kwa kuwashambulia watu wazaifu.
8Sehemu mbili za tatu za watu katika inchi zitaangamizwa;
ni sehemu moja ya tatu tu itakayobaki.
9Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki,
nitaipima na kuitakasa,
kama vile mutu anavyosafisha feza,
kama vile wanavyopima zahabu.
Halafu wao wataniomba mimi,
nami nitawajibu.
Nitasema: Hawa ni watu wangu,
nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.