1Katika mwaka wa makumi mbili na tatu wa utawala wa mufalme Yoasi wa Yuda, Yoahazi mwana wa Yehu alianza kutawala Israeli, akaendelea kutawala akiwa kule Samaria kwa muda wa miaka kumi na saba.
2Alitenda maovu mbele ya Yawe. Alitenda zambi sawa na Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi. Hakuacha kutenda zambi hii.
3Yawe alikasirika, akawafanya watu wa Israeli washindwe katika vita mara kwa mara na mufalme Hazaeli wa Aramu na mwana wake Beni-Hadadi.
4Yoahazi akamusihi Yawe, naye Yawe alipoona jinsi mufalme wa Aramu alivyowatesa watu wa Israeli akasikia maombi yake.
5Yawe akawapa Waisraeli kiongozi ambaye aliwakomboa kutoka kwa Waaramu. Halafu wakakaa kwa amani kama vile walivyokuwa zamani.
6Hata hivyo hawakuacha zambi za mufalme Yeroboamu ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi; lakini waliendelea na zambi zao na sanamu ya Ashera ilibakia kule Samaria.
7Yoahazi hakukuwa na waaskari, lakini alikuwa tu na wapanda-farasi makumi tano, magari kumi na waaskari wa miguu elfu kumi. Hii ilikuwa ni kwa sababu mufalme wa Aramu alikuwa ameyaangamiza makundi ya waaskari ya Israeli na kuyakanyaga chini kama mavumbi.
8Mambo mengine ya Yoahazi, yote aliyofanya na ushujaa wake yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.
9Yoahazi akakufa na kuzikwa kule Samaria, naye mwana wake Yoasi akakuwa mufalme kwa pahali pake.
Mufalme Yoasi wa Israeli10Katika mwaka wa makumi tatu na saba wa utawala wa mufalme Yoasi wa Yuda, Yoasi mwana wa Yoahazi alianza kutawala Israeli akiwa kule Samaria, na akatawala kwa muda wa miaka kumi na sita.
11Yoasi vilevile alitenda maovu mbele ya Yawe. Hakuacha zambi zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi. Aliendelea kuzitenda.
12Mambo mengine ya Yoasi, yote aliyofanya na ushujaa wake katika vita alivyopigana na mufalme Amazia wa Yuda, yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Israeli.
13Yoasi akakufa na kuzikwa katika makaburi ya kifalme kule Samaria, naye mwana wake Yeroboamu akatawala kwa pahali pake.
Kifo cha Elisha14Nabii Elisha alipata ugonjwa ambao ulimwua. Alipokuwa karibu kufa, mufalme Yehoasi wa Israeli alimutembelea. Alipomufikia Elisha, akalia, akisema: “Baba yangu, baba yangu! Ulikuwa wa lazima kuliko magari ya Israeli na wapanda-farasi wake!”
15Elisha akamwamuru: “Ulete upinde na mishale!”
Yoasi akavileta.
16Elisha akamwambia ajitayarishe kupiga mishale. Mufalme akajitayarisha na Elisha akaiweka mikono yake juu ya mikono ya mufalme.
17Mufalme alifuata maagizo ya nabii na kufungua dirisha ambalo lilielekea Aramu. Elisha akatoa amri: “Tupa mushale!” Mara tu mufalme alipotupa mushale, nabii akasema: “Wewe ndio mushale wa Yawe, ambao kwa njia yake atapata ushindi juu ya Waaramu. Utapigana na Waaramu kule Afeki mpaka uwashinde.”
18Halafu Elisha akamwambia mufalme atwae mishale mingine na kuipiga chini. Mufalme akapiga mishale chini mara tatu, kisha akaacha.
19Elisha akakasirika sana, akamwambia mufalme: “Mbona haukupiga mara tano au sita? Hivyo ungewaangamiza Waaramu kabisa. Lakini sasa utawashinda mara tatu tu.”
20Elisha akakufa, naye akazikwa.
Kila mwaka, makundi ya Wamoabu yalikuja kuishambulia inchi ya watu wa Israeli.
21Siku moja, wakati wa mazishi, watu waliona moja kati ya makundi yale. Wakatupa maiti katika kaburi la Elisha na kukimbia. Mara tu maiti hiyo ilipogusa mifupa ya Elisha, ilifufuka na kusimama wima.
Vita kati ya Israeli na Aramu22Mufalme Hazaeli wa Aramu akawatesa sana watu wa Israeli wakati wote wa utawala wa Yoahazi.
23Lakini Yawe aliwarehemu na kuwaonea huruma. Aliwaangalia kwa wema kwa sababu ya agano lake na Abrahamu, Isaka na Yakobo. Hakuwaangamiza wala hajawaachilia hata kidogo mpaka leo.
24Hazaeli mufalme wa Aramu alipokufa, Beni-Hadadi mwana wake akatawala kwa pahali pake.
25Mufalme Yoasi akamushinda Beni-Hadadi mara tatu na kuikomboa miji yote iliyotekwa wakati wa utawala wa Yoahazi, baba ya Yoasi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.